» » Lowassa Mikononi mwa Polisi Leo........Ni Kufuatia Wito wa DCI Aliyemtaka Afike Polisi saa Nne

Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania, Edward Lowassa ametakiwa kuripoti katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) leo  saa nne asubuhi.

Lowassa ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) amepewa wito huo kwa njia ya barau bila kuelezwa sababu za yeye kutakiwa kufanya hivyo.

Msemaji wa CHADEMA, Tumaini Makene na Lowassa mwenyewe wote wamethibitisha kupata taarifa za wito huo huku wakisema si chama wala mhusika anayejua sababu za kuitwa.

Aidha, katika mahojiano aliyofanya Lowassa na The Citizen kwa njia ya simu, amesema kuwa anadhani kuitwa kwake kuna uhusiano na kauli aliyoitoa mwishoni wa juma wakati wa futari kuhusu Masheikh wa Uamsho.

Lowassa alimtaka Rais Magufuli kuingilia kati suala hilo ambapo Masheikh kadhaa wanashikiliwa kwa zaidi ya miaka minne sasa bila maendeleo yoyote ya tuhuma zinazowakabili. Masheikh hao ambao walikamatwa Zanzibar wanatuhumiwa kwa ugaidi ambapo Lowassa alitaka Rais aingilie kati ili kesi hiyo iweze kusikilizwa.

“Sina hakika kama hii ndio sababu, lakini nahisi tu. Ila ukweli utafahamika  nitakapokutana na DCI,”  alisema Lowassa kwenye mahojiano hayo ya simu.


Tuma picha/ habari what-sap 0769436440

BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS

tupe maoni yako

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles