Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma anatarajiwa kuzuru nchini Tanzania hii leo katika ziara ya rasmi ya siku tatu kufuatia mwaliko wa rais John Pombe Magufuli.
Akizungumza na vyombo vya habari siku ya Jumatatu Waziri wa maswala ya kigeni nchini Tanzania Augustine Mahiga alisema kuwa ziara hiyo inalenga kuimarisha uhusiano wa kibiashara mbali kuangazia maswala mbali mbali ya maendeleo.
Rais Zuma ataandamana na mawaziri sita pamoja na wafanyibiashara kadhaa kutoka Afrika Kusini.
- Zuma adaiwa kusinzia bungeni
- Waandamanaji wanakusanyika kumpinga Zuma
- Jacob Zuma : Siogopi kufungwa jela
- Rais wa zamani Afrika Kusini ampinga Jacob Zuma
Atakuwa nchini humo kuanzia tarehe 10 hadi 13 akitarajiwa kufanya mazungumzo na mwandalizi wake rais Magufuli katika ikulu ya rais.
Kulingana na Mahiga kiwango cha biashara kati ya mataifa hayo mawili kimeongezeka kutoka dola milioni 803 mwaka 2006 hadi dola bilioni 2.2 2016 hatua iliobuni ajira 20,916.
Tuma picha/ habari what-sap 0769436440
BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI



No comments:
Post a Comment