» » Msitarajie Wenger ajiuzulu Arsenal’ Lauren.

Beki wa zamani wa Arsenal Lauren

Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionLauren alijiunga na Arsenal kutoka Mallorca mwaka 2000 na akawachezea mechi 159 ligini kwa miaka sita
Shinikizo hazitamlazimisha meneja wa muda mrefu wa Arsenal Arsene Wenger ajiuzulu, beki wa zamani wa klabu hiyo Laurena mesema.
Arsenal watakutana na Southampton katika Ligi ya Premia Jumatano jioni na iwapo watashinda huenda wakapanda hadi nafasi ya tano.
Mkataba wa Mfaransa huyo unafikia kikomo mwisho wa msimu huu na amekosolewa sana msimu huu kutokana na matokeo ya klabu hiyo.
Lauren, 40, aliambia BBC Africa: "Anafahamu kukabiliana na presha, natumai kwamba mambo yatakuwa sawa hivi karibuni."
Lauren alichezea Arsenal mechi 159 ligini kati ya 2000 na 2007 na alikuwa kwenye kikosi kinachosifiwa sana cha "invincibles" (Wasioshindwa) ambacho kilishinda taji la ligi mwaka 2003-2004.
Beki huyo wa kulia wa zamani wa Cameroon alisema: "Sidhani (Wenger) atajiuzulu. Amekabiliwa na shinikizo kwa miaka 30-35, akisimamia klabu kubwa zinazokabiliwa na presha."
Februari, Wenger alisema angeamua kuhusu mkataba mpya Machi au Aprili lakini baadaye alisema labda alifanya kosa kwa kuahidi watu kwamba angekuwa ameamua hatima yake katika kipindi hicho.

Tuma picha/ habari what-sap 0769436440


BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS


tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...