» » Haya hapa Matokeo ya uchaguzi wa wabunge wa CHADEMA Bunge la Afrika Mashariki

Bunge la Tanzani jana limepiga kura na kuwachagua wabunge wawili wa CHADEMA watakaoungana na wenzao 7 kutoka CUF na CCM kwa ajili ya kuiwakilisha Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki (EALA).

Uchaguzi huo wa wabunge wa CHADEMA ulirudiwa jana baada ya wagombea wa kwanza kukataliwa bungeni kwa kupigiwa kura ya hapana kwa kile kilichoelezwa kuwa hawakuwa wamekidhi vigezo.

Katika uchaguzi wa jana, wabunge wawili waliochaguliwa ni  Josephine Sebastian Lemoyan na Pamela Pamela Maasay.

Katika kinyang’anyiro hicho wagombea wengine walikuwa nia Ezekiel Wenje, Lawrence Masha, Salum Mwalimu na Prof. Safari.

==>Matokeo ni kama ifuatavyo;
1.Abdallah Safari- kura 35.
2-Wenje -kura 34
3-Lawrence Masha -kura 44
4-Salim Mwalimu -kura 54
5- Josephine Lemoyan -kura 219
6-Pamela Maasay kura -200.

Kufuatia ushindi wa wagombea hao wawili, wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki sasa wanafikia 9 ambapo 5 ni wanawake na 4 ni wanaume.

==>Wabunge tisa wa Tanzania katika Bunge las Afrika Mashariki ni;
  1.     Fancy Nkuhi (CCM)
  2.     Happiness Legiko (CCM)
  3.     Maryam Ussi Yahya (CCM)
  4.     Dkt Abdullah Makame (CCM)
  5.     Dkt Ngwaru Maghembe (CCM)
  6.     Alhaj Adam Kimbisa (CCM)
  7.     Habib Mnyaa (CUF)
  8.     Josephine Sebastian Lemoyan (CHADEMA)
  9.     Pamela Pamela Maasay (CHADEMA).


Tuma picha/ habari what-sap 0769436440


BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS

tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...