» » Trump abadili msimamo kuhusu NATO na kusema shirika hilo sasa linafaa

Trump abadili msimamo kuhusu NATO na kusema shirika hilo sasa linafaa

Trump amesema kuwa shirika hilo sasa lina umuhimu baada ya kuanza kukabiliana na ugaidi
Image captionTrump amesema kuwa shirika hilo sasa lina umuhimu baada ya kuanza kukabiliana na ugaidi
Rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa shirika la kujihami la NATO sasa linafaa na kwamba halijapitwa na wakati hatua ambayo imewashangaza washirika wake.
Akizungumza na katibu mkuu wa shirika hilo Jens Stoltenberg katika Ikulu ya Whitehouse ,Trump amesema kuwa tishio la ugaidi limesistiza umuhimu wa muungano huo.
Ametoa wito kwa NATO kusaidia washirika wake nchini Iraq na Afghanistan.
Bwana Trump mara kwa mara amekuwa akitilia shaka umuhimu wa shirika hilo huku akilalamika kwamba Marekani inatoa kitita kikubwa cha ufadhili wake ikilinganishwa na mataifa mengine.
Sio mara ya kwanza kwa bwana Trump kulalamika kuhusu shirika hilo siku ya Jumatano.
Katika mahojiano na jarida la Wall Street alisema kuwa hataitaja China kuwa imekuwa ikishawishi sarafu yake ili kuangazia maslahi yake ,licha ya kuahidi kusema hivyo siku moja tu baada ya kuchukuwa mamlaka.
Katika mahojiano ya pamoja ya vyombo vya habari na Stoltenberg Bwana Trump alisema: katibu mkuu wa Nato na mimi tumefanya mazungumzo ya kufana kuhusu ni nini zaidi NATO inaweza kufanya katika vita dhidi ya ugaidi.
Nililalamika kuhusu hilo hapo awali na wakafanya mabadiliko na sasa wanakabiliana na ugaidi.
Nilisema NATO 'imepitwa na wakati' lakini sasa 'haijapitwa na wakati'.
Bwana Trump alisisitiza wito wake kwa wanachama wa NATO kuchanga fedha zaidi kwa shirika hilo.
Tuma picha/ habari what-sap 0769436440


BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.sn.news&hl=en

tupe maoni yako

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles