» » MASOMO YA VIJANA KUTOKA KATIKA KITABU CHA CHAGUWA MAISHA SOMO LA KWANZA

Kutokana na uhitaji wa Elimu ya maisha kwa vijana 4sn news utakuwa inakupatia masomo ya ndoa mahusiano kutoka Kwenye nukuu na vitabu mbali mbali hivyo wambie vijana wako marafiki zako ndugu na jamaa was Downlod bApps ya 4sn news IPO play store/Android ili wapate masomo hayo bure kabisa Kwenye Simu zao

SoMo la leo
CHAGUWA MAISHA SEHEM YA KWANZA

Andrew,  David  na  Peter  walilitazama  kwa  makini  lori  lililokuwa  likipita  kijijini  mwao. “Unajua,”  Andrew  aliwaambia  rafiki  zake,  "naomba  niwe  na  gari  siku  moja.    Nitapenda  kuendesha gari  kila  mahali.    Sijui  itanilazimu  kuwa  na  misimu  mingapi  ya  mavuno  ili  niweze  kupata  fedha  za kununua  gari  dogo  la  mizigo  nianze  kufanya  biashara" "Mimi  sipendi  kupata  gari  dogo  la  mizigo,"  David  alijibu.    "Ndoto  yangu  ni  kuendelea  na  masomo hadi  Chuo  Kikuu  ili  niwe  Daktari.    Nimeshuhudia  vile  wazazi  wangu  walivyohangaika  kupata chakula na karo ya shule.  Nawaheshimu kwa kazi yao kubwa, nawashukuru kwa vile walivyojitolea mhanga  ili  sisi  watoto  wao  tusome.    Lakini  sipendi  kufanyakazi  shambani  kutwa  nzima  kama  wao. Ningependa  niwe  na  zahanati  ili  niweze  kuwasaidia  wananchi  na  wakati  huo  huo  niweze  kuisadia familia  yangu." "Hilo  ni  wazo  zuri  sana  David,"  Peter  alisema.    "Lakini  mimi  sipendi  kusoma  tu  kila  wakati. Tutakapofuzu  masomo  yetu  ya  shule  ya  upili  mwaka  ujao,  sitaendelea  na  masomo  tena.    Sipendi kuachana  na  maisha  ya  mashambani.    Ninaipenda  sana  milima  hii,  hapa  ndipo  ningependa  kuishi. Ndoto  yangu  ni  kuwa  na  nyumba  nzuri,  mke  anayenipenda,  watoto  sita  pamoja  na  kundi  la ng'ombe.    Iwapo  nitakuwa  na  hivi  vyote,  nitakuwa  na  furaha  ya  ajabu." "Lakini,"  Peter  aliendelea  kusema,  "Alex  yuko  wapi?    Sijamwona  kwa  majuma  kadhaa  sasa." "Hujui?"    Andrew  alijibu.    "Alilazimika  kukatisha  masomo  yake,  kwa  sababu  familia  yake  haikuwa na  uwezo  wa  kumlipia  karo  ya  shule.    Baba  yake  ameugua  kwa  muda  mrefu  na  hali  yake  imekuwa mbaya  zaidi.    Hivi  sasa  familia  inatumia  fedha  yote  kwa  ajili  ya  matibabu  yake.    Alex  hajui  maisha yake  ya  baadaye  yatakuwa  vipi.    Alikuwa  akiongoza  katika  somo  la  hesabu  darasani  mwetu  na amekuwa  akitarajia  kuwa  mara  tu  amalizapo  shule  ya  upili,  atachukua  kosi  ya  komputa.    Angependa pia  kuwa  mhasibu.    Lakini  iwapo  baba  yake  atafariki,  ana  mashaka  kama  ataendelea  na  masomo  yake, na  atakabiliwa  na  jukumu  kubwa  la  kuwatunza  mama  yake,  ndugu  na  dada  zake."

MAMBO YAKUJADILIANA 1)

Vijana  hawa  walikuwa  na  ndoto  gani? 2) Kila  kijana  alitakiwa  kufanya  uchaguo  gani  ili  kutimiza  ndoto  yake? 3)  Ni  uchaguo  gani  ungewasaidia  kuepuka  na  mambo  yasiyoweza  kuwafanya  watimize ndoto  zao? 4) Unafikiri  kuwa  Alex  anaweza  kutimiza  ndoto  zake  endapo  baba  yake  atafariki?    Ikiwa ndiyo,  anaweza  kutimiza  kwa  njia  gani?  

KESHO LITAENDELEA.

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles