» » Mke wa Mwanamuziki, Roma Mkatoliki akielezea tukio kutekwa kwa Mumewe na jitihada alizozichukua.

Mke wa Mwanamuziki, Roma Mkatoliki akielezea tukio kutekwa kwa Mumewe na jitihada alizozichukua.

Mke wa Roma Mkatoliki, Nancy ambaye ni mama wa mtoto mmoja aitwae Ivan, amedai yeye pamoja na ndugu zake wameshazunguka kila sehemu bila mafanikio kumtafuta mume wake ambaye ametekwa usiku wa Jumatano hii akiwa studio za Tongwe Record Masaki jijini Dar es Salaam.

Akiongea na waandishi wa habari jana jioni, Nancy alisema mara ya mwisho kuzungumza na Roma ilikuwa juzi saa kumi na mbili jioni.

“Mimi kama mke wa Roma mara ya mwisho niliwasiliana na mume wangu juzi saa kumi na mbili jioni, akaniambia anaelekea Tongwe Records kwajili ya kazi zake za kila siku. Baada ya hapo sikuwa nampata tena kwenye simu lakini nikachukulia ni kawaida tu simu imezima, nimekuja kuamka saa 7 nikapokea simu kutoka kwa rafiki yake akaniambia uko na Roma nikamwambia hapana alikuwa Tongwe, akaniambia kuna taarifa kwenye mitandanao na mimi nikaingia nikakuta hizo taarifa kama walizopata watu wengine,” alisema Nancy na kuongeza:

“Baada ya hapo nikaanza kutafuta watu wa kunisaidia, baadhi ya ndugu zangu wameangaika vituo vyote vya polisi Roma hayupo, hadi sasa hivi sifahamu yuko wapi, kwa ufupi sina ninachokijua wala ninachokifahamu. Jitihada zangu za kutafuta kwenye vituo vyote vya polisi nimemaliza,”

Alisema mume wake huyo hakuwai kumpatia taarifa yoyote kama anatafutwa na polisi wala ana tatizo na mtu yeyote.

Pia aliwaomba wadau mbalimbali pamoja na watanzania kwa ujumla kumuunga mkono katika jitihada za kumtafuta mume wake ambaye mpaka sasa hajulikani aliko.

Kamanda wa Polisi Kanda ya Dar es salaam Kamishna Simon Sirro amesema kuwa wamezipata taarifa hizo na wanazifanyia kazi.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...