Mgomo kutishia biashara ya mafuta Nigeria
AFP
Madereva wa Malori yanayobeba mafuta nchini Nigeria wanatarajiwa kuwa na mgomo siku ya Jumatatu.
Chama cha wafanyakazi wa Petroli na Gesi asili nchini humo kimesema watagoma kupinga mishahara midogo na barabara mbovu ambazo zinaharibu magari yao.
Msemaji wa chama cha wafanyakazi, Cogent Ojobo, ameonya kutokea kwa upungufu wa Petroli, Dizeli na mafuta ya taa nchi nzima wakati huu ambapo usambazaji utasitishwa.
Ojobo amesema hakuna tarehe ya mwisho wa mgomo iliyoelezwa
Tuma picha/ habari what-sap 0769436440
BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.sn.news&hl=en
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

No comments:
Post a Comment