» » Marekani kuchukua wakimbizi 1200 kutoka Australia

Marekani kuchukua wakimbizi 1200 kutoka Australia


Donald Trump na waziri mkuu wa Australia Turnbull
Image captionDonald Trump na waziri mkuu wa Australia Turnbull
Makamo wa rais wa Marekani, Mike Pence, amethibitisha kuwa Marekani itatimiza ahadi iliyotolewa na rais msataafu, Rais Obama, kwamba Marekani itapokea wakimbizi 1200 kutoka kambi za wakimbizi nchini Australia.
Akizungumza baada ya mazungumzo na waziri mkuu wa Australia, Malcolm Turnbull, mjini Sydney, Bwana Pence alisema, wale wanaotaka hifadhi Marekani, watakabiliwa sheria kali za ukaguzi.
Makubaliano hayo kuhusu wakimbizi, yalisababisha mzozo kwenye simu baina ya Bwana Turnbull na Rais Trump mwezi wa Februari, ambapo Rais Trump alielezea makubaliano hayo kuwa ya kijinga.
Bwana Pence alisema Marekani itachunguza makubaliano hayo, lakini itayatekeleza, kwa sababu ya kuheshimu umuhimu wa urafiki kati ya nchi mbili hizo.

Tuma picha/ habari what-sap 0769436440

BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS

tupe maoni yako

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles