» » Aliyeshambulia Urusi anatoka Asia ya Kati

Aliyeshambulia Urusi anatoka Asia ya Kati

Haki miliki ya pichaREUTERSImage captionRais Vladmiri Putin wa Urusi akiweka maua kwenye eneo palipotokea mlipuko

Vikosi vya usalama nchini Urusi wako kwenye taadhari kubwa baada ya kutokea milipuko kwenye vituo viwili vya treni ya chini ya ardhi mjini St Petersburg.

Milipuko hiyo ilisababisha watu 11 kupoteza maisha na zaidi ya watu 40 walijeruhiwa.

Wachunguzi nchini Urusi wamelichukulia tukio hilo kuwa ni shambulio la kigaidi. Vyombo vya habari vimeripoti vikinukuu vyanzo vya usalama vikisema milipuko hiyo huenda imelipuliwa na mtu aliyejitoa muhanga kutoka eneo la Asia ya Kati.

Kifaa kingine kilichokutwa kwenye stesheni nyingine kiliteguliwa na wataalam wa kutegua mabomu.

Rais Vladmir Putin yuko St.Petersburg kupata maelezo ya wataalam wa masuala ya usalama, pia aliweka mashada ya maua kuwakumbuka walioathirika kwenye ajali hiyo, amesema ni mapema mno kujua chanzo cha tukio hilo lakini uchunguzi unafanyika.

''Sababu ya tukio hilo haijafahamika, hivyo ni mapema kuzungumzia kuhusu hilo.uchunguzi utaonyesha , lakini maelezo yote yatatizamwa, ilikupata sababu ya ajali hiyo na sababu ya uhalifu huo, juuu ya yote ugaidi, tutaona, uchunguzi utatupa majibu yote kuhusu kilichotokea.'' alieleza Putin

Mshirikishe mwenzako

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles