» » SOMO: KESHA LA ASUBUHI

KESHA LA ASUBUHI

ALHAMISI-MARCHI 2, 2017

*SUALA LA KUFA NA KUPONA*

*"Akasema,niache,niende,maana kunapambazuka,akasema,sikuachi,usiponibariki." MWANZO 32:26*

▶Akiwa katika zahama kuu ya maisha yake,Yakobo alienda pembeni kusali.Alikuwa amejazwa na kusudi moja lililomtawala kabisa-kutafuta badiliko la tabia.

▶Ilikuwa kwenye eneo pweke la kwenye milima,makazi ya wanyama wa porini na maficho ya wanyang'anyi na wauaji. Akiwa mpweke na bila ulinzi,Yakobo aliinamia nchi katika dhiki yake kuu....Alitoa sala yake kwa Mungu huku akilia machozi kwa uchungu. Ghafla akashikwa na mkono wenye nguvu. Akadhani kuwa adui alikuwa anataka kumuua na akajaribu kujikwapua kutoka mkononi mwa mvamizi.

▶Pale gizani,hawa wawili walipambana ili kupata ushindi.Hakuna neno lililotamkwa,lakini Yakobo alitumia nguvu zake zote na alijitahidi muda wote. Alipokuwa akipambana hivyo kwa ajili uhai wake,hisia ya hatia iliugusa moyo wake;dhambi zake ziliinuka mbele yake zikimtenga na Mungu. Lakini katika hali yake hii mbaya ya kutisha,alikumbuka ahadi za Mungu na moyo wake wote ukaelekezwa kusihi apate rehema.

▶Pambano liliendelea hadi karibu kuche,wakati huyu mgeni alipoweka kidole chake kwenye paji la Yakobo na akalemaa mara ile. Ndipo mzee huyu wa imani alipotambua aina ya hasimu zake. Akajua kwamba alikuwa katika  pambano na mjumbe wa kimbingu na ndio sababu jitihada yake (Yakobo) ambayo haikuwa ya kawaida kibinadamu haikuweza kumpatia ushindi.  Huyu alikuwa Kristo,"Malaika wa Agano",ambaye alikuwa amejidhihirisha kwa Yakobo. Mzee huyu wa imani sasa alikuwa amelazwa na akiugulia maumivu makali,lakini hakuacha kumshikilia....

▶Yule mgeni alisihi,"niache,niende,maana kunapambazuka",lakini Yakobo akajibu akasema,"sikuachii,usiponibariki". Kama huu ungekuwa ujasiri unaotokana na majivuno,ufidhuli,Yakobo angeangamizwa mara moja;lakini namna ya Yakobo ilikuwa ni uhakika wa ungamo la kutostahili,huku akitumainia uaminifu wa Mungu anayetunza agano.

▶Kile Yakobo alichokipigania kwa nguvu zake mwenyewe bila mafanikio aliweza kukipata kupitia kwa kujitoa nafsi na imani thabiti.

*TAFAKARI NJEMA, UBARIKIWE*

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...