» » Nnauye: Waziri aliyefutwa asema bado anaunga mkono juhudi za Magufuli

Nnauye: Waziri aliyefutwa asema bado anaunga mkono juhudi za Magufuli


Nnape NauyeHaki miliki ya pichaNNAPE NAUYE/TWITTER
Aliyekuwa waziri wa habari, utamaduni, Sanaa na michezo nchini Tanzania Nape Nnauye amesema bado anaunga mkono juhudi za Rais John Magufuli katika kujaribu kufanikisha mageuzi nchini humo.
Bw Nnauye, akizungumza wakati wa kukabidhi rasmi afisi kwa mrithi wake Dkt Harrison Mwakyembe, kadhalika amesema ataendelea kushirikiana na wizara hiyo.
Amesema yeye ni mdau mkubwa katika sekta zilizomo chini ya wizara hiyo.
Bw Nnauye alifutwa kazi wiki iliyopita siku moja baada yake kupokea ripoti ya kamati ya uchunguzi kuhusu uvamizi uliotekelezwa na mtu anayedaiwa kuwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda katika studio za kituo cha habari cha kibinafsi cha Clouds.
Kamati hiyo, kwenye ripoti yake, ilionekana kumkosoa Bw Makonda na kusema alitumia vibaya mamlaka yake.
"Heshima aliyonipa mheshimiwa Rais ni kubwa mno na nitaendelea kumuunga mkono katika dhamira yake njema ya kuleta mageuzi nchini," alisema Bw Nnauye, kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa wizara ya habari na michezo Tanzania.
Taarifa hiyo inasema Bw Nnauye ameahidi ataendelea kuwa mtiifu kwa Rais Magufuli, serikali na Chama cha Mapinduzi (CCM).
Bw Nnauye akikabidhi rasmi afisi kwa Dkt MwakyembeHaki miliki ya pichaHABARI MAELEZO, TANZANIA
Image captionBw Nnauye akikabidhi rasmi afisi kwa Dkt Mwakyembe
Bw Nnauye, ambaye ni mbunge wa Mtama, alisimamia wizara hiyo kwa miezi 15.
Waziri mpya Dkt Mwakyembe amesema anategemea kuendelea kupata ushirikiano kutoka kwa Bw Nnauye.

Mada zinazohusiana

Tuma picha/ habari what-sap 0769436440

BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.sn.news&hl=en

tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...