Makamu wa rais Afrika Kusini akosoa kufutwa kazi waziri wa fedha
Hivi ni viunganisho vya nje na vitafungua katika dirisha mpyaSambaza habari hii Facebook Sambaza habari hii Twitter Sambaza habari hii Messenger Sambaza habari hii Email Mshirikishe mwenzako
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionBwana Ramaphosa (kushoto) alisema kuwa hatajiuzulu
Makamu wa rais nchini Afrika Kusini Cyril Ramaphosa ameitaja hatua ya kufutwa kazi waziri wa fedha Pravin Gordhan kuwa isiyokubalika.
Kufutwa kazi kwa Gordhana kumesababisha masoko ya hisa kushuka kwa asilimia 5.
Bwana Gordhan alionekana kama mpinzani mkubwa wa ufisadi kwenye uongozi ambao umekosolewa vikali.
Aikuwa mmoja wa mawaziri waliofutwa kazi wakati Rais Jacob Zuma, alilifanyia mabadiliko baraza la mawaziri.
Zuma amfukuza kazi waziri wa fedha Pravin GordhanDonald Trump na Uhuru Kenyatta wazungumza kwa Simu
Bwana Ramaphosa alikiambia kituoa cha habari cha SABC kuwa hatajiuzulu kufuatia kufutwa kwa mawaziri hao bali ataendelea kuwatumikia watu.
Haki miliki ya pichaAFPImage captionMr Gordhan remained defiant in the wake of his sacking
Pravin Gordhan alitajwa na wengi kama mtu mwenye tajriba ya kusimamia uchumi.
Alikuwa akizuia matumizi makubwa ya serikali na kukataa wito wa rais wa kutaka matumizi ya serikali kuongezwa.
Huu ndiyo duru ya pili bwana Gordhan anahudumu kama waziri wa fedha baada ya kuhudumu kwanza kati ya mwaka 2009 na 2014.
Zuma azuiwa kuhudhuria mazishi ya KathradaWageni wajihami Afrika Kusini kujilinda
Aliteuliwa mwaka 2015 kuchukua mahala pa David van Rooyen. Uteuzi wa bwana Van Rooyen ulikumbwa na utata na alihudumu kama waziri wa fedha kwa muda wa wiki moja.
Haki miliki ya pichaSOUTH AFRICA GOVERNMENTImage captionCyril Ramaphosa, Jacob Zuma na Pravin Gordhan wakati wa siku ya kusomwa bajeti mwezi uliopita
Mshirikishe mwenzako

No comments:
Post a Comment