» » Mahakama yazuia marufuku mpya ya Trump Marekani

Mahakama yazuia marufuku mpya ya Trump Marekani

Haki miliki ya pichaAFPImage captionMaandamano yamefanyika Marekani kupinga marufuku hiyo

Mahakama moja katika jimbo la Hawaii imezuia utekelezaji wa marufuku mpya ya usafiri iliyokuwa imetangazwa na Rais Donald Trump.

Marufuku hiyo ilizuiwa saa chache kabla ya kuanza kutekelezwa saa sita usiku Alhamisi.

Jaji Derrick Watson alisema ushahidi uliotolewa na serikali katika kutetea marufuku hiyo ni wa kutiliwa shaka.

Trump hajui apeleke wapi mshahara wakeMaswali magumu kuhusu marufuku ya Trump

Serikali ilikuwa imejitetea mahakamani ikisema marufuku hiyo inalenga kuimarisha usalama wa taifa.

Rais Trump ameeleza uamuzi huo wa jaji kuwa wa kushangaza na akasema mahakama imevuka mpaka.

Agizo lililokuwa limetolewa na Trump, ambalo lilifaa kuanza kutekelezwa usiku wa kuamkia leo, ungepiga marufuku kwa miezi mitatu raia kutoka nchi sita zenye Waislamu wengi kuzuru Marekani.

Mataifa hayo ni Iran, Libya, Syria, Somalia, Sudan na Yemen.

Aidha, ingezuia wakimbizi kuingia Marekani kwa kipindi cha siku 120.

Bw Trump amesisitiza kwamba hatua hiyo inalenga kuzuia magaidi wasiingie Marekani lakini wanaoipinga wamesema inabagua makundi ya watu.

Kwa nini Trump hataendesha gari tena

Marufuku nyingine ya awali aliyokuwa ameitoa Januari ilisababisha mtafaruku na maandamano kabla ya kuzuiwa na jaji mjini Seattle.

Akihutubu katika mkutano wa hadhara mjini Nashville, Tennessee Jumatano jioni, Bw Trump alisema uamuzi huo wa jaji mjini Hawaiii uliifanya Marekani "kuonekana dhaifu".

Alisema ataendelea na kesi hiyo "hadi itakapofikia", ikiwemo kwenda Mahakama ya Juu.

ALiongeza: "Tutashinda."

Haki miliki ya pichaREUTERSImage captionPresident Trump told a rally in Nashville that he would fight the court ruling

Hawaii ni mojawapo ya majimbo kadha ya Marekani yanayopinga marufuku hiyo.

Sababu zilizosababisha Trump Kushinda

Mawakili wa jimbo hilo waliambia mahakama kwamba marufuku hiyo inakiuka katiba ya Marekani kwamba watu hawafai kubaguliwa kwa misingi ya asili yao.

Jimbo hilo pia limesema marufuku hiyo itaathiri utalii na uwezo wa serikali ya jimbo hilo kupokea wanafunzi na wafanyakazi kutoka mataifa ya nje.

Mada zinazohusiana

Donald TrumpMarekani

Mshirikishe mwenzako

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles