» » Gari la Uber linalojiendesha lahusika katika ajali Marekani

Gari la Uber linalojiendesha lahusika katika ajali Marekani

Image captionMagari ya UBER

Gari moja linalojiendesha kutoka kampuni ya Uber limepata ajali kwa kugongana na gari lingine huko nchini Marekani katika jimbo la Arizona,

Picha zimeonyesha gari hilo likiwa limepinduka lakini bado hakuna taarifa zozote za majeruhi.

Kituo kimoja cha televisheni kimeripoti kuwa dereva wa gari lililohusika katika ajali na gari la Uber hakuipisha gari hiyo.

Hatahivyo haijulikani iwapo gari hilo la Uber lilikuwa kwenye mfumo wa kuendeshwa bila dereva au la .

Huduma hiyo ya kampuni ya Uber ya magari yanayojiendesha bila dereva ilianza safari zake za uchukuzi mjini Arizona mwezi uliopita, ikiongeza uchukuzi wa safari hiyo kwenye miji mengine kama vile Pittsburgh na San Francisco.

Kampuni za kiteknologia zinafanya harakakti za kuboresha huduma hiyo ya usafiri wa magari yasiyo na madereva kwa lengo la kumiliki biashara hiyo ambayo thamani yake inakadiriwa kukuwa na kufikia bilioni ishirini katika kipindi cha miaka 10 ijayo.

Mshirikishe mwenzako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...