» » » Eneo ambapo watoto hupewa majina ya kustaajabisha

Eneo ambapo watoto hupewa majina ya kustaajabisha





Katika eneo moja mashariki mwa Zambia mwandishi wa BBC Chris Haslam, anakumbana na kijana mdogo ambaye anajikakamua kusukuma baiskeli kubwa ambayo imebeba mitungi ya maji, kuni na mfuko wa mchele.
Kwa vile kijana anaisukuma baiskeli hiyo na mikono yake miwili, hana njia ya kuwafukuza nzi kutoka kwa macho yake.
Jina lake ni "Mulangani". Jina hilo ni la jamii ya Nguni linalomaanisha "niadhibu" au yule ambaye ni lazima adhibiwe. Chris Haslam alimuuliza dereva kuhusu ni nani anayeweza kumpa mtota wake jina baya kama hilo?
"Labda babu yake au chifu," dereva akajibu. Nchini Zambia na hata Zimbabwehasa mashambani , ni jambo la kawaida wazazi kuwaalika wazee wa jamii kuwapa majina watoto wanapozaliwa.
Mara nyingine chifu huwa anataka kuiadhibu familia, anasema dereva, "au anafikiri kuwa mtoto aliyezaliwa ni mzigo kwa familia."


Lakini kijana huyo si peke yake aliye na jina la kutisha. Baadaye anakutana na "Chilumba", jina linalomaansiha "kaburi la ndugu yangu"
Kisha anakutana na Balaudye - "nitaliwa" na Chakufwa- "amekufa"
Pia anakutana na Daliso linalomaanisha "baraka" na Chikondi linalomaanisa "upendo".
Kwenye utamaduni wa Afrika kuna tabia ya kuwapa watoto majina kutokana na nyakati walizozaliwa, kwa mujibu wa Clare Mulkenga afisa wa huduma za watoto nchini Zambia.
Anasema kuwa hata hivyo ni vyema kwa wale wanaozaliwa nyakati nzuri lakini pia huwa ni bahati mbaya kwa wengine.



http://www.bbc.com/swahili

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...