» » » » » » DIAMOND AULA UBALOZI WA BIDHAA ZA GSM

DIAMOND AULA UBALOZI WA BIDHAA ZA GSM

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii 

Msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul (Diamond Platnum) amekuwa Balozi wa Bidhaa za GSM na kuwataka watanzania wanunue bidhaa hizo kuacha kutumia gharama kwa kufuata nje ya nchi. 

Akizungumza leo na waandishi wa habari, Diamond amesema kuwa licha ya kuwa balozi katika bidhaa za GSM ameweza yeye kununua kutokana vitu mbalimbali katika maduka hayo. 

Amesema kuwa GSM walikuwa na uwezo wa kutafuta wasanii wa nje ya nchi lakini wakaona kuna umuhimu wa kuwatumia wasaani wa ndania kama mabalozi katika bidhaa zao. 
 
"Hivyo katika hilo na kuchangia maendeleo kwa wasanii wetu wa hapa nyumbani,wanaojituma na kuonesha mafanikio yao makubwa kwa kile wanachokifanya,sisi kama GSM tumeamua kutimia msanii Diamond Plutnum kuwa Balozi wa bidhaa zetu" alisema

Aidha amesema kuwa ubalozi huo utafanya kutangaza muziki wake kwa mashabiki wa ndani na wan je ya nch. Diamond amesema kuwa balozi hakuadhiri ubalozi mwingine kutokana kuwa kinachotangazwa ni bidhaa ambazo haziingiliani. 
 
 Msanii wa Bongo Fleva,  Nasibu Abdul (Diamond Platnum) akizungumza na waandishi habari baada ya kukabidhiwa ubalozi wa bidhaa za GSM leo jiiini Dar es Salaam.
 Afisa Masoko wa GSM, Lauma Mohammed  akizungumza na waandishi wa habari juu ya Diamond kuwa Balozi wa Bidhaa za GSM leo jijini Dar es Salaam.
 Waandishi wa habari wakimsikilizwa Msanii wa Bongo Fleva,  Nasibu Abdul (Diamond Platnum)  hawapo pichani leo jijini Dar es Salaam. 

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...