• HQ
  • MKOA
  • WILAYA
  • IDARA
  • contact

4SN NEWS

NYAYO ZA MATUMAINI

Home » News » Angalia Kiangazi kilivyo hatarisha maisha nchini Kenya

Angalia Kiangazi kilivyo hatarisha maisha nchini Kenya

IVST TANZANIA Mar 14, 2017 0 No comments

Kiangazi chahatarisha maisha nchini Kenya


Zaidi ya watu milioni 2 wameathirika kutokana na kiangazi kinachoendelea kukumba maeneo mengi nchini Kenya na kusababisha maafa kwa binadamu na mifugo.
  • Maelfu ya mifugo wameaga dunia kutokana na kiangazi.BBC
    Mfugaji asimama kando ya mifupa ya mifugo wake waliofariki kutokana na kiangazi kinachoendelea katika kijiji cha Watiti, Moyale kaunti ya Marsabiti kaskazini mwa Kenya. Maelfu ya mifugo wamekufa kutokana na ukosefu wa maji na lishe
  • Mifugo katika kaunti ya Marsabit wanaishi kwa maji pekee.BBC
    Wafugaji wamzingira ngombe aliyekufa baada ya kuisha nguvu karibu na bwawa la maji lililobaki na maji katika eneo la Ambalo, Moyale, kaunti ya Marsabit.
  • Maelfu ya watu wanateseka kutokana na ukosefu wa maji na chakula katika kaunti ya Marsabit, wengine wakivuka mpaka hadi Ethiopia kutafuta maji na chakulaBBC
    Zaidi ya watu milioni 2 wameathiriwa na kiangazi kutokana na ukosefu wa mvua tangu mwishoni mwa mwaka uliopita. Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ametangaza kiangazi kuwa janga la kitaifa na kuomba msaada wa kimataifa.
  • Inawabidi wanawake kutembea umbali wa zaidi ya kilomita kumi kutafuta maji.BBC
    Wanawake wengi wanakesha kwenye maeneo machache yaliyobaki na maji wakisubiri nafasi ya kuteka maji, na wanasafiri umbali mrefu kuelekea visimani na kurudi nyumbani.
  • Mifugo ni kitega uchumi kwa jamii za wafugaji kaskazini mwa Kenya, na kwa sasa wamepata hasara kubwa. Bei ya mifugo pia imeanguka kwa kiwango kikubwaBBC
    Zaidi ya 95% ya mabwawa ya maji yamekauka katika eneo Moyale kaunti ya Marsabit. Wafugaji wanasafiri umbali mrefu kutafuta maji, wengine wakivuka mpaka kuelekea Ethiopia kutafuta maji
  • Mifugo wengi wamekufa kutokana na ukosefu wa chakula na maji, pamoja na kutembea umbali mrefu kutafuta maji na lishe.BBC
    Katika kijiji cha watiti eneo la MOyale, wafugaji wanagawana chakula chao cha nyumbani na mifugo kutokana na ukosefu wa lishe. Mifugo wengi wamekufa kutokana na ukosefu wa chakula na maji, pamoja na kutembea umbali mrefu kutafuta maji na lishe.
  • Shirika la Word Vision limekuwa likiendeleza miradi ya kutoa huduma za maji katika maeneo mbalimbali yaliyokumbwa na kiangazi.BBC
    Mfanyikazi wa shirika la uhisani World Vision katika mojawepo wa bwawa lililokauka katika eneo la Moyale. Bwawa hili lilikuwa tegemeo la zaidi ya ffamilia mia tano na maelfu ya mifugo.
  • Wafugaji wana hofu kwamba mifugo wao wataangamia bwawa hili la Badan Rero likikauka. Zaidi ya mifugo laki moja huletwa hapa kila siku.BBC
    Maelfu ya mifugo wanategemea mabwawa machache yaliyobaki na maji katika kaunti ya Marsabit na huenda mifugo hawa wakafa iwapo mvua inayotarajiwa kunyesha mwezi Aprili itakosa kunyesha.
  • Ukosefu wa maji umesababisha vifo vya mifugo wengi na wafugaji wanalalamika kwamba serikali imewatelekeza.BBC
    Mifugo ni kitega uchumi kwa jamii za wafugaji kaskazini mwa Kenya na zaidi ya 80% hutegemea kipato kutokana na mauzo ya mifugo. Kaunti ya Marsabit ina mifugo zaidi ya milioni 4.
  • Mvua fupi zilizokuwa zikitarajiwa katika maeneo ya kasakzini mwa Kenya zilifeli na kusababisha kiangazi kikubwa kinachotishia kusababisha maafa nchini KenyaBBC
    Mvua fupi zilizotarajiwa kunyuesha katika maeneo ya kasakzini mwa Kenya zilifeli na kusababisha kiangazi kikubwa kinachotishia kusababisha maafa nchini Kenya
  • Kiangazi kimesambaratisha familia nyingi katika kaunti ya Marsabit ambapo watu wanahamahama wakitafuta maeneo yaliyo na maji na lishe, watoto wakiachwa na mababu.BBC
    Kiangazi kimesambaratisha familia nyingi katika kaunti ya Marsabit ambapo watu wanahamahama wakitafuta maeneo yaliyo na maji na lishe, watoto wakiachwa na mababu.
  • Maisha ya binadam pia huenda yakaangamia katika kaunti ya Marsabit na kaunti zingine zilizo karibu kama vile Turkana.BBC
    Inatabiriwa kwamba maelfu ya wanyama watakufa iwapo mvua itaendelea kuadimika katika kipindi cha wiki chache zijazo. Maisha ya binadam pia huenda yakaangamia katika kaunti ya Marsabit na kaunti zingine zilizo karibu kama vile Turkana.
  • Mifugo wanaishi kwa maji pekee, kwani ardhi imegeuka vumbi. Wafugaji wana hopfu kwamba iwapo maji yataisha basi mifugo wao wataangamia.BBC
    Mifugo wanaishi kwa maji pekee, kwani ardhi imegeuka vumbi. Elijah Chiwe anayesimamia shirika la uhisani la World Vision kaunti ya Marsabit, anasema hali huenda ikadorora iwapo wadau hawatachukua hatua ya kudumu ya kukabiliana na hali hii.

Mshirikishe mwenzako

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Share !

Topics: News

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post
Newer Post Older Post Home

No comments:

Post a Comment

Subscribe to: Post Comments (Atom)

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles

  • Angela Merkel aahirisha mkutano wake na Trump Marekani
    Angela Merkel aahirisha mkutano wake na Trump Marekani Haki miliki ya picha AFP Image caption Kuna baridi kali katika jiji la N...

C. E.O - GASTO ALEX DIDAS

C. E.O - GASTO ALEX DIDAS
+255769436440 Mwanza Tanzania

Popular Posts

  • JUA STYLE 7 MPYA ZA KUFANYA MAPENZI ILI MPENZI WAKO AWEZEKUSHIKA MIMBA FASTER
    1.Kufanya mapenzi katika mtindo (style) ambayo itafanya mbegu za kiume zikae kwa muda mrefu ukeni na hivyo nyingi kupand...
  • WENYEVITI WA MITAA DAR WAJIVUA MADARAKA HUKU WAKIMZOMEA MKUU WA WILAYA..!!!
    WENYEVITI 400 na wajumbe 130 wa serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam wamejivua madaraka kwa kutoshiriki kutoa huduma kwenye mitaa yao, ...
4SN NEWS © 2026. All Rights Reserved.

Designed by IVST TANZANIA +255615866660

Total Pageviews