USHINDI HATIMAYE - SIKU NGUMU SANA MAISHANI
MHUBIRI: Mchungaji David Mbaga
MAHALI: Kanisa la Waadventista Wasabato Mabatini Mwanza
WADHAMINI: Chama cha Wajasiriamali na Wanataalum(ATAPE) wakishirikiana na Kanisa la Waadventista Wasabato Mabatini.
WADHAMINI: Chama cha Wajasiriamali na Wanataalum(ATAPE) wakishirikiana na Kanisa la Waadventista Wasabato Mabatini.
MAFUNGU: 1 Samwel 21:1-9; Waruni 1:17; Warumi 3:10, Warum 6:23; 2 Petro 3:9; Mathayo 12:3-7; Kutoka 34:6, 7
Hofu haipaswi kuwa sehemu ya maisha ya muumini, jinsi gani mtu anaishinda wasiwasi? Mungu anatueleza tumpe woga wetu wote na wasiwasi. Kwa nini Mungu Anataka kutubebea matatizo yetu? ni kwa sababu Yeye(MUNGU) anatujali.
Sisi imetupasa kumpa Mungu matatizo yetu,ameahidi kutupa amani ipitayo uwezo wetu wote. lazima tulete mahitaji yetu yote na wasiwasi kwa Mungu katika maombi badala ya kujisumbua kwayo.Woga ukitawala utakusababisha kutumia njia zako mwenyewe maishani.
Kuna kuogopa endapo utasahau kule Mungu alikokutoa.Tusitumie juhudi zetu wenyewe ili kumpendeza Mungu.Je! utalipa nini ili usamehewe na Mungu? Tujifunze kwa Daudi ambaye aligundua amekosa,Msamaha ni bure. Woga unaondoka katika maisha yako kwa Yesu aliyekuja katika mwili. Yesu amemharibu Shetani aliyetutawala kwa woga wa mauti, Akatuacha huru.
Tambua dhambi zako,Mwite Yesu!Katika maisha watu wengi hukwama kutatua changamoto zao wanapokuwa kwenye hali ngumu za kimaisha,twapasa kupaza sauti kwa neno lolote TUSIKATE TAMAA ,bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru haja zenu na zijulikane na Mungu.
Kuruhusu kutawaliwa na woga, ni kumfanya Mungu kuwa na uwezo mdogo kuliko yale yanayotuogopesha.Hatupaswi kuyaogopa makumi elfu ya watu, waliojipanga juu yetu pande zote, TUSIKANYAGE VITU VITAKATIFU.MUNGU hapendi mtu yeyote apotee, akikusamehe anakupatia AMANI YA MOYO; BWANA AKUBARIKI
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
No comments:
Post a Comment