USHINDI HATIMAYE- SAULI MATATANI
MHUBIRI: Mchungaji David Mbaga
MAHALI: Kanisa la Waadventista Wasabato Mabatini Mwanza
Mafungu:1 Samwel 28:3-13; 1 Samwel 25:1;Mhubiri 9:5-6,10; 1Thesalonike 4:13-16; Mwanz 2:7
MAHALI: Kanisa la Waadventista Wasabato Mabatini Mwanza
Mafungu:1 Samwel 28:3-13; 1 Samwel 25:1;Mhubiri 9:5-6,10; 1Thesalonike 4:13-16; Mwanz 2:7
Wewe unapokutana na adui unakimbilia wapi?Sauli alipokuwa akiona maadui alitetemeka na kutafuta waganga na wachawi ili watengeneze mambo yake.Mambo yakiwa magumu subiri miguuni pa Yesu mpaka amekutendea jambo.
WALIO KUFA WANAJUA LOLOTE?
Biblia inasema kwamba wafu “hawajui lolote kamwe.” Pia, inasema kwamba wafu ‘hawajiwezi katika kifo.’ (Mhubiri 9:5).Neno la Mungu linaeleza hivi: “Mungu akamfanya mtu kutoka katika mavumbi ya nchi na kupuliza katika mianzi ya pua yake pumzi ya uhai, naye mtu akawa nafsi hai.”(Mwanzo 2:7).
Biblia inasema kwamba wafu “hawajui lolote kamwe.” Pia, inasema kwamba wafu ‘hawajiwezi katika kifo.’ (Mhubiri 9:5).Neno la Mungu linaeleza hivi: “Mungu akamfanya mtu kutoka katika mavumbi ya nchi na kupuliza katika mianzi ya pua yake pumzi ya uhai, naye mtu akawa nafsi hai.”(Mwanzo 2:7).
Sisi ni viumbe tulioumbwa kutokana na mavumbi tunapokufa, mawazo yetu yanapotea. Lazaro alipofufuliwa hakusema chochote kuhusu hali yake alipokuwa mfu, kwa kuwa wafu hawajui lolote. Shetani ndiye anayeendeleza uwongo kwamba nafsi haiwezi kufa na inaweza kuwadhuru walio hai. Hata hivyo, watu wanaoiamini Biblia wanalindwa wasipotoshwe na uwongo kama huo. Wamekuja kujua ukweli wa kwamba Shetani anajaribu kuwadanganya watu waamini wafu wanaweza kuwasiliana na walio hai.(Zaburi 115:17,2Petro 2:4,Kumb la 18:10,11)
KUNA AINA MBILI KUU ZA UFUFUO:
i)Ufufuo wa kwanza au ufufuo wa uzima. Wote waliolala katika Bwana watafufuliwa kwanza. Kufumba na kufumbua miili yao itabadilishwa tena na kuungana na wale walio hai ambao nao miili yao itabadilishwa na kuwa ya utukufu, kisha wote kwa pamoja watakwenda kumlaki Bwana Yesu mawinguni.
i)Ufufuo wa kwanza au ufufuo wa uzima. Wote waliolala katika Bwana watafufuliwa kwanza. Kufumba na kufumbua miili yao itabadilishwa tena na kuungana na wale walio hai ambao nao miili yao itabadilishwa na kuwa ya utukufu, kisha wote kwa pamoja watakwenda kumlaki Bwana Yesu mawinguni.
ii) Ufufuo wa hukumu au ufufuo wa aibu ambao ni ufufuo wa watenda mabaya au wenye dhambi wote. Baada ya kufufuliwa watahudhuria wote mbele ya kiti cha enzi, kikubwa, cheupe cha hukumu. Yesu Kristo mhukumu wa haki atawaonyesha waziwazi matendo yao maovu.Biblia inasema katika Ufunuo 20:5,11-15). Pumzi ya Mungu ikitoka mwili unarudi mavumbini,hauna kazi tena.Ikiwa unadukuduku,ugomvi na mtu,uadui,chuki,makwazo ni vema mkamaliza naye akiwa hai usingoje akafa utakuwa umechelewa Yesu ndiye mafanikio ya kweli ni Mungu anayejali mpelekee shida zako zote yuko tayari kukupa msaada HATIMAYE USHINDI.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
No comments:
Post a Comment