» » USHINDI HATIMAYE FEBRUARI 12, 2017- MUNGU ANAPO NYAMAZA KIMYA

USHINDI HATIMAYE FEBRUARI 12, 2017- MUNGU ANAPO NYAMAZA KIMYA






MHUBIRI: Mchungaji David Mbaga
MAHALI: Kanisa la Waadventista Wasabato Mabatini Mwanza
WADHAMINI: Chama cha Wajasiriamali na Wanataalum(ATAPE) wakishirikiana na Kanisa la Waadventista Wasabato Mabatini.

MAFUNGU: 1 Samwel 28:6,7; 1Samwel 8 :6,7,10,18,19; 1Samwel 16:1-2
“Siku ile itakapowadia, mtalia kwa kutaka msaada kutokana na mfalme mliyemchagua, naye BWANAhatawajibu.”(1 Samwel 8:19)
Je umewahi kutafuta kuijua sababu ya Mungu kutojibu maombi au unaongeza tu kuomba? Kumbuka maombi siyo yanayomsukuma Mungu kujibu ila imani yetu. Je unaomba sawasawa na mapenzi ya Mungu au unaomba kutokana na tamaa yako?
Mungu si kama jini unaloliita kukutimizia lolote unalotaka. Mungu hajibu maombi yanayopingana na mapenzi, au matakwa yake yanayopatikana katika Biblia.
Inawezeka na wewe umeombea hitaji lako kwa muda mrefu na huoni majibu, umetubu DHAMBI,Nakwambia sababu ya kutokujibiwa ulichokuwa unaomba utendewe hakikuwa mpango wa Mungu lakini MUNGU atabaki kuwa MUNGU jifunze kurudi kwa Mungu kumuuliza usilalamike.
Mtumishi wa Mungu-Sauli,alikuwa kwenye shida, na akaenda mbele za Mungu kumuomba amsaidie, lakini Biblia inasema Mungu akakaa kimya, Baada ya kuona Mungu hamjibu,akageukia pepo.Dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone,hata hataki kusikia.Bwana anasema tukitafuta njia yetu wenyewe BWANA HATA SIKIA
Iko neema ya kutosha kwani katika mafanikio yako,taabu yako elewa kuna mtu/watu wanakuombea. BWANA ana hitaji watu jasiri wa kuikataa dhambi,shujaa wa Bwana Daudi mwana wa Yese. Hatutakiwi kushindwa; Tafuta nguvu ya Mungu kutosha kuleta ushindi! Amen

Habari kwa hisani ya Kirumba Seventh-day Adventist Church

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...