Sunday, February 12, 2017
RATIBA YA USHINDI HATIMAYE
11:00-12:00 Majadiliano kabla ya mkutano
12:00-12:30 Uimbaji
12:30-01:00 Kaya na familia
01:00-01:15 Uimbaji
01:15-02:00 Mahubiri makuu
.
Mahubiri ya Ushindi hatimaye yamezinduliwa tarehe 11.02.2017 ndani ya kanisa la Waadventista wa Sabato Mabatini jijini Mwanza.Mahubiri hayo yamezinduliwa rasmi na msaidizi wa mwenyekiti uinjilisti wa Divisheni ya mashariki na kati mwa Afrika Mch Joel Okindo.Waliohudhuria pia ni Viongozi mbalimbali wa Konferensi ya South Nyanza ,Union ya Kaskazini na kusini mwa Tanzania.
Ushindi hatimaye itaendelea kukujia kwa muda wa jumla ya siku ishirini na moja kila siku sa 12:00 hadi 02:00 usiku.Endelea kualika ndugu,rafiki na jamaa katika nyumba na makanisa yetu ili kushiriki mibaraka ya mkutano huu.Ubarikiwe
|
Kwaya ya Buswelu sda katika ufunguzi wa mkutano huu hapo jana walitubariki na nyimbo zao za kutumia gita/ mpingo. |
|
Mchungaji Semba mmoja wa wanenaji katika ufunguzi wa mkutano huu hapo jana akihudum kwenye masomo ya kaya na familia ndoa na mahusiano, kipindi chake ni cha kwanza kabisa usikose kipindi chake kinaanza saa 12:30 usikose kabisa. |
picha ya Rock City Mwanza
|
Katibu mkuu wa NTUC Mchungaji Makoye aliposimama na kusema jambo katika ufunguzi wa mkutano huu hapo jana. |
|
Mchungaji Mmbaga mmoja wa wanenaji katika mahubiri ya USHINDI HATIMAYE katika ufunguzi wa mkutano huu hapo jana alikuwa na somo zuri sana lililo tuonyesha jinsi ambavyo Daudi alimshinda Goliati akiwa nikijana mdogo . |
|
Timu ya wachungaji k na maafisa wa kanisa la waadventista wa Sabato katika picha ya pamoja katika ufunguzi wa mkutano huu hapo jana. |
Tuma picha/ habari what-sap 0769436440
tupe maoni yako
Pakua App Yetu-Bofya Hapa
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
No comments:
Post a Comment