» » Mourinho: Wayne Rooney anaweza kuondoka Manchester United

Mourinho: Wayne Rooney anaweza kuondoka Manchester United

Wayne RooneyHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionRooney amekuwa Manchester United tangu 2004
Meneja wa Manchester United Jose Mourinho amesema bado inawezekana Wayne Rooney aihame klabu hiyo mwezi huu.
Mshambuliaji huyo wa England mwenye umri wa miaka 31 alifunga bao lake la 250 United mwezi uliopita na kuwa mchezaji aliyefunga mabao mengi katika historia ya klabu hiyo.
Hata hivyo, kumekuwa na uvumi kwamba huenda akahamia China.
Soko la kuhama kwa wachezaji Ligi Kuu ya China litafungwa wiki ijayo.
Mourinho aliulizwa iwapo nahodha huyo wa United atakuwa Old Trafford kufikia wakati huo.
"Itabidi mumwulize mwenyewe," Mourinho alisema.
"Bila shaka siwezi kuwahakikishia (kwamba atakuwa hapa). Siwezi kuwahakikishia kwamba nitakuwa hapa wiki ijayo, nitawezaje kuwahakikishia kwamba mchezaji atakuwa hapa msimu ujao?"
Mkataba wa Rooney United ni wa hadi 2019 na majuzi alikuwa amedokeza kwamba kuna uwezekano huenda asimalize muda wote huo United.
Amekuwa hapewi nafasi ya kuwa katika kikosi cha kuanza mechi msimu huu na amefunga mabao matano pekee.
Hata hivyo, Mourinho alisema Oktoba kwamba Rooney hakuwa anenda "popote" na alisisitiza Jumanne kwamba hataki mchezaji huyo aihame Manchester United.
"Siwezi kumsukuma - au kujaribu kumsukuma - nyota wa klabu hii ahame," aliongeza Mourinho.
"Hivyo, itabidi mumwulize iwapo anaona kama atakuwa katika klabu hii kipindi kilichosalia cha uchezaji wake au iwapo anadhani atahama.
"Si swali langu hilo kwa sababu ninafurahia kuwa naye. Sitaki aondoke."
Tuma picha/ habari what-sap 0769436440

tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...