» » Rais wa Guinea achaguliwa kuwa Mwenyekiti Mpya wa Umoja wa Afrika (AU)

Rais wa Guinea achaguliwa kuwa Mwenyekiti Mpya wa Umoja wa Afrika (AU)

Rais wa Guinea, Alpha Conde amechaguliwa leo kuwa Mwenyekiti mpya wa Umoja wa Afrika (AU), uchaguzi uliofanyika katika vikao vya viongozi wa nchi wanachama vinavyoendelea katika Makao Makuu ya umoja huo mjini Addis Ababa nchini Ethiopia.

Rais Conde anapokea uongozi kwa Rais wa Chad Idris Deby ambaye alikuwa ndiye kiongozi wa umoja wa hadi.

Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika ni kiongozi asiye na maamuzi (ceremonial head of the Union). Mwenyekiti huyu huchaguliwa  na Marais wa Nchi wanachama wa AU ambaye hushika wadhifa huo kwa mwaka mmoja tu. Uongozi huu huenda wa zamu katika Kanda tano za bara la Afrika (Kaskazini, Kusini, Mashariki, Magharibi, na Afrika ya Kati).

Nafasi hii ilianzishwa mwaka 2002 ambayo Rais Mstaafu wa Afrika Kusini, Thabo Mbeki ndiye alikuwa mwenyekiti wa kwanza.

Rais wa Chad,  Idriss Deby (kushoto) akikabidhi madaraka kwa Mwenyekiti mpya wa Umoja wa Afrika, Rais Alpha Conde wa Guinea (kulia).
Asante kwa kutembelea Blog yetu washirikishe na wenzako, Pia tunaomba maoni yako hapa WHATSAP (+255) 0769436440 Karibu Sana Read More

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...