» » Maharusi wafunga ndoa kwa kutumia dola moja Kenya

Maharusi wafunga ndoa kwa kutumia dola moja Kenya

Wilson Muturi na mkewe Ann
Image captionWilson Muturi na mkewe Ann walitumia dola moja pekee wakati wa harusi yao
Ushawahi kuona sherehe ya harusi isiyo na burudani wala mapochopocho na gharama husika haizidi dola moja?
Basi wiki hii, Wakenya, Wilson Mutura na Ann walitumia shilingi mia moja au dola moja tu kufunga ndoa. Dola yenyewe ilitumika kununua pete mbili zilizogharimu shilingi mia moja.
Sherehe hiyo tulivu ilifanyika katika mtaa wa Kasarani, mjini Nairobi.
Walipoona kuwa uhusiano wao ulinoga kwa kudumu kwa zaidi ya miaka mitatu na kuwa ni heri waiweke iwe rasmi, Wilson Mutura na Ann Mutura walianza safari ya kufunga pingu za maisha. Lakini safari yenyewe ilikumbwa na changamoto za kifedha.
Kutokana na mazoea ya sherehe za kifahari nchini humo, wawili hao walipanga na kupangua sherehe hiyo kwa sababu hawakuweza kukusanya kiwango walicholenga cha dola mia tatu.
Maombi yao kwa familia na marafiki kuwafanyia mchango, hayakutimizwa.
Hilo liliwafanya waahirishe sherehe hiyo mara tatu.
"Nilipozungumza na kakangu, aliniambia, kwa nini nijisumbue ilhali wengi wao hawakuhitaji sherehe ya harusi?" aliuliza.
Lakini baada ya muda, Bwana harusi, Wilson, hakuwa na la kufanya ila kumshawishi mpenzi wake kuhusu uwezo wake.
"Wilson aliponieleza hali yake, sikukataa. Mapenzi yetu yalizidi yote," anasema bi Harusi, Ann.
Harusi ya dola moja Kenya yasisimua wengi
Ingawa walikuwa na uwezo wa kuishi kwa mtindo wa 'come we stay' uliomaarufu kwa vijana wengine ambapo wapenzi wanaishi pamoja bila kuoana, Wawili hao walikwenda kwa askofu Jasper Owach kutoka Kanisa la Community Christian worship centre mjini Nairobi kurasmisha harusi yao.
"Mapenzi yetu yalidumu kwa muda na ili kujistiri kutoka maovu baada ya kupata baraka ya wazazi, tuliamua kufanya mambo yetu rasmi," anasema Wilson.
Siku yenyewe ilipofika, bwana Harusi, Wilson aliwashangaza waumini baada ya kukimbia nje sherehe ikiendelea.
"Alitoka ghafla kununua pete ya harusi nilipokuwa naendelea na shughuli ya kuwafunganisha," alisema askofu Jasper Owach, ambaye aliongoza hafla hiyo.
Wilson alirejea na walipokuwa wanatamka kauli za ndoa, Wilson alitoa pete hizo zilizofungwa kwa gazeti na wakavikana pete.
Wanandoa waliofanya harusi ya shilingi za kenya 100
Image captionWilson na Anne wamelipiwa fungate na kampuni ya Bonfire
Kwa sasa wawili hao, wamewarai vijana kutozuiwa na uwezo wao wa kifedha na hivyo basi kuhalalisha mapenzi yao kupitia ndoa.
Kutokana na hatua yao, wawili hao, wamelipiwa fungate na kupewa zawadi na Wakenya waliovutiwa na ndoa hiyo ya dola moja.
Bila kutarajia, mwishowe harusi yao imekuwa ya 'kifahari'.

Mada zinazohusiana

Asante kwa kutembelea Blog yetu washirikishe na wenzako, Pia tunaomba maoni yako hapa WHATSAP (+255) 0769436440 Karibu Sana Read More

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...