» » Lukuvi awapania viongozi walevi wa madaraka

Lukuvi awapania viongozi walevi wa madaraka


Iringa. Waziri wa Nyumba, Ardhi na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amesema chanzo cha migogoro inayolikabili Taifa kwa sasa hususan wakulima na wafugaji,  imetokana na kukosekana kwa mipango bora ya matumizi ya ardhi, huku viongozi wa serikali za vijiji wakibadilisha matumizi bila kushirikisha wananchi.
Alitoa kauli hiyo wakati akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi hati 810 za kimila za kumiliki ardhi kwa wakazi wa Kijiji cha Kinywang’anga, Wilaya ya Iringa mkoani hapa.
 “Tumejifunza kutokana na uzoefu tuliopata, migogoro mingi ya ardhi imetokana na baadhi ya  viongozi wetu wa serikali za vijiji ambao wamekuwa wakibadilisha matumizi ya ardhi bila kufuata utaratibu,” alisema.
Lukuvi alisema Serikali haitasita kuwafuta kazi viongozi  wa serikali za vijiji watakaobainika kujihusisha kubadili  mpango wa matumizi bora ya ardhi za vijiji bila ya kushirikisha wananchi.
Alisema licha ya kuwaondoa kwenye nafasi zao, viongozi hao watakamatwa na kufikishwa katika  vyombo vya sheria kwa tuhuma za matumizi mabaya  ya madaraka.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, Mkurugenzi Msaidizi wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID),  Dan Thompson alisema wanaendesha miradi ya aina hiyo kwenye vijiji 41 vya mikoa ya Iringa na Mbeya kupitia Mradi wa Feed the Future.
Habari zaidi soma Gazeti la Mwananchi

Asante kwa kutembelea Blog yetu washirikishe na wenzako, Pia tunaomba maoni yako hapa WHATSAP (+255) 0769436440 Karibu Sana Read More

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...