» » Kijana wa Miaka 22 Alivyombaka Mtoto wa Miaka 5 Karibu na Ziwa Victoria..!!!

Kijana aliyejulikana kwa jina la Petro Magayane miaka 22 mkazi wa Igombe Jijini Mwanza anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kosa la kumbaka na kumjeruhi katika sehemu zake za siri mtoto mwenye umri wa miaka 5 ambaye ni mkazi wa eneo hilo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza DCP Ahmed Msangi amesema kuwa tukio hilo limetokea tarehe 23.01.2017 majira ya saa 2 usiku katika kijiji cha Igombe “A” kata ya Bugogwa wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza.
Inadaiwa kuwa mtuhumiwa akiwa amelewa  alifika maeneo ya nyumbani anapoishi mtoto huyo kisha akamtuma dukani maeneo ya mwaloni Igombe.
Aidha baada ya muda mchache kupita mtuhumiwa alimfuata mtoto huko dukani kisha kumfanyia ukatili wa kumbaka na kusababisha majeraha na maumivu makali katika sehemu za siri za mtoto huyo.
Wananchi walitoa taarifa polisi kuhusiana na tukio hilo, askari walifika eneo la tukio na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo ambaye yupo katika mahojiano na jeshi la polisi, pindi uchunguzi ukikamilika atafikishwa mahakamani.
Msangi amesema kuwa uchunguzi wa awali unaonesha chanzo cha tukio hili ni ulevi. Mtoto amepatiwa matibabu hospitali na hali yake inaendelea vizuri.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...