» »Unlabelled » Geert Wilders: Mashitaka yangu yanachochewa na chuki za kisiasa

Geert Wilders: Mashitaka yangu yanachochewa na chuki za kisiasa


Wilders amesema ana haki ya kuongelea matatizo ya nchi hiyo
Image captionWilders amesema ana haki ya kuongelea matatizo ya nchi hiyo
Geert Wilders ambaye ni Kiongozi wa chama tawala, kinachopinga uislam nchini Uholanzi ameiambia mahakama kwamba mashtaka yake yanachochewa na chuki za kisiasa chafu pamoja na ubaguzi wa rangi.
Katika kipindi cha Televisheni alipokuwa akisomewa mashtaka yake mara ya mwisho, ameeleza kuwa mahakama haitamhukumu yeye peke yake bali itawahukumu mamilioni ya wanaume kwa wanawake nchini Uholanzi.
Kiongozi huyo amesema ana haki ya kuongelea matatizo ya nchi hiyo ikiwemo kupunguza idadi ya wananchi wa Morocco wanaoishi nchini humo.
Mashtaka hayo yamesababishwa na uchochezi wa kiongozi huyo ambapo alisikika akiwauliza wafuasi wake kama wanataka idadi ndogo ya wamorocco wanaoishi Nchini humo huku wafuasi wake walisikika wakishangilia na kujibu, idadi chache! Chache!
Uholanzi inatarajia kufanya uchaguzi mkuu mwezi wa tatu mwakani na baadhi ya kura za maoni zinapendekeza bwana Wilders, na chama cha uhuru kikiongoza.
Asante kwa kutembelea Blog yetu washirikishe na wenzako, Pia tunaomba maoni yako hapa au tupigie kwa (+255) 0769436440 Karibu Tena

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles