John Kerry akwama kwenye foleni Delhi, India
Mshirikishe mwenzako
Wageni mashuhuri wanapozuru mji wa Delhi, hutarajia kupata barabara zikiwa wazi namna hii.
Lakini kwa raia wa kawaida, barabara huwa hivi...
... na hali huwa mbaya zaidi wakati wa mvua ya upepo wa msimu.
Lakini Waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry alipofika Delhi kwa mashauriano na maafisa wa serikali Jumatatu jioni, hakuwa na bahati.
Mvua kubwa ilinyesha na 'kukosa kutambua cheo chake'.
Badala ya magari yake kupitia barabara zilizo wazi, msafara wake wa magari ulikwama kwenye foleni zaidi ya saa moja.
Lilikuwa jambo lisilo la kawaida kwa sababu maafisa wa usalama huondoa magari barabarani kutengeneza njia ya kutumiwa na wageni mashuhuri.
Watu kwenye mitandao ya kijamii walianza kufanyia mzaha masaibu hayo ya Bw Kerry. Baadhi, kama Karthik hapa alipendekeza Bw Kerry afanye wafanyavyo wenyeji mvua ikinyesha.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
No comments:
Post a Comment