IGP MANGU kukabidhiwa uenyekiti SARPCCO
Mkuu wa jeshi la polisi nchini Inspekta Jenerali wa Polisi IGP ERNEST MANGU anatarajia kukabidhiwa uenyekiti wa Shirikisho la wakuu wa Majeshi ya Polisi
Mkuu wa jeshi la polisi nchini Inspekta Jenerali wa Polisi IGP ERNEST MANGU anatarajia kukabidhiwa uenyekiti wa Shirikisho la wakuu wa Majeshi ya Polisi kusini mwa Afrika, SARPCCO wakati wa mkutano utakaofanyika Septemba 16 mwaka huu jijini Arusha.
Kwa mujibu wa tarifa iliyotolewa na jeshi la polisi nchini, IGP MANGU atakabidhiwa uenyekiti huo kutoka kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi la MSUMBIJI na atadumu katika nafasi hiyo kwa mwaka mmoja.
Tarifa hiyo imeeleza kuwa Mkutano huo utatanguliwa na mkutano wa siku mbili wa kamati tendaji za SARPCCO ambazo zitaandaa ajenda na mapendekezo yatakayowasilishwa katika mkutano wa wakuu wa Polisi.
Mkutano huo pamoja na mambo mengine utajadili namna ya kukabiliana na uhalifu wa kuvuka mipaka na kuweka mikakati na maazimio ya kufanya Oparesheni za pamoja za kupambana na uhalifu
Pia mkutano huo utajadili utekelezaji wa maazimio mbalimbali kupitia kamati tendaji za wakurugenzi wa upelelezi, kamati tendaji ya sheria, kamati tendaji ya mafunzo na kamati tendaji ya mtandao wa Polisi wanawake.
SARPCCO iliundwa mwaka 1995 kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa Majeshi ya Polisi kwa nchi za kusini mwa Afrika katika kukabiliana na uhalifu yenye nchi KUMI na TANO ikiwemo TANZANIA
Kwa mujibu wa tarifa iliyotolewa na jeshi la polisi nchini, IGP MANGU atakabidhiwa uenyekiti huo kutoka kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi la MSUMBIJI na atadumu katika nafasi hiyo kwa mwaka mmoja.
Tarifa hiyo imeeleza kuwa Mkutano huo utatanguliwa na mkutano wa siku mbili wa kamati tendaji za SARPCCO ambazo zitaandaa ajenda na mapendekezo yatakayowasilishwa katika mkutano wa wakuu wa Polisi.
Mkutano huo pamoja na mambo mengine utajadili namna ya kukabiliana na uhalifu wa kuvuka mipaka na kuweka mikakati na maazimio ya kufanya Oparesheni za pamoja za kupambana na uhalifu
Pia mkutano huo utajadili utekelezaji wa maazimio mbalimbali kupitia kamati tendaji za wakurugenzi wa upelelezi, kamati tendaji ya sheria, kamati tendaji ya mafunzo na kamati tendaji ya mtandao wa Polisi wanawake.
SARPCCO iliundwa mwaka 1995 kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa Majeshi ya Polisi kwa nchi za kusini mwa Afrika katika kukabiliana na uhalifu yenye nchi KUMI na TANO ikiwemo TANZANIA
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

No comments:
Post a Comment