DALILI TATU ZINAZOONYESHA MTU ATAKAYECHELEWA KUFANIKIWA.
1)Mtu ambaye yuko bize tangu asubuhi kufanya mambo mbalimbali, lakini katika hayo hakuna chochote anachofanya kinachochangia kumsaidia kupiga hatua kuelekea katika malengo yake makuu aliyonayo.
2)Mtu ambaye watu wote wanaomzunguka wana uwezo mdogo wa mawazo,kifedha na kiufahamu wa mambo mbalimbali. Kiufupi yeye ndiye bora kuliko wote wanaomzunguka na hafanyi juhudi kuzungukwa na watu walio juu Zaidi yake.
3)Mtu ambaye kile alichokuwa anakijua mwanzoni mwa mwaka hakina tofauti na kile ambacho anakijua leo.Kiufupi ni kuwa hajaongeza maarifa yoyote katika yale ambayo amekuwa nayo siku Zote.Ukiona siku hadi inaisha haujajifunza kitu kipya ujue unaelekea kushindwa katika malengo yako.
UNATAKA KUFANIKIWA?ZIEPUKE DALILI HIZI.
See You At The Top.
www.JoelNanauka.com

No comments:
Post a Comment