» »Unlabelled » Mmoja wa makamanda wa IS auawa nchini Syria

Mmoja wa makamanda wa IS auawa nchini Syria


Abu Muhammad al Adnani
Image captionAbu Muhammad al Adnani
Kundi la wapiganaji la Islamic state limetangaza kuwa mmoja wa kamanda wake mwandamizi ambae ni msemaji wa kundi hilo, Abu Muhammad al-Adnani ameuwawa nchini Syria.
Taarifa ya mtandao unaohusiana na kundi hilo Amaq, inasema kuwa Abu Muhammad ameuwawa wakati alipokuwa kwenye operesheni za kijeshi katika jimbo la Allepo.
Mtandao huo haukutoa taarifa nyengine zaidi.
Wanajeshi wa marekani wamethibitisha kuwa walikuwa wamemlenga Abu Muhammad al-Adnani lakini wanasema bado walikuwa wakichunguza matokeo ya shambulizi la anga la siku ya Jumanne katika mji wa Al-Bab, kaskazini mashariki ya jimbo la Allepo.
Marekani inamuelezea Abu Muhammad al-Adnani kuwa ni mpangaji mkuu wa mashambulizi ya nje ya I-S na imesema kuwa kifo chake kinaweza kuwa nukta muhimu ya kushindwa kwa kundi hilo.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...