» »Unlabelled » JINSI YA KUNUNUA BIDHAA MTANDAONI



VITU VYA KUZINGATIA
·         Kuficha credential zako mf. Neno au namba ya siri, habari zako binafsi (personal particulars)
Jambo muhimu kukumbuka wakati wa kununua vitu online ni kuhakikisha unaficha habari zako za kibenki, kwani kuna wizi mkubwa kwa kutumia mtandao!, watu wamekuwa pia wanafungua tovuti feki ili kuwalaghai watu!. Pia jaribu kutafuta habari tofauti tofauti kujua athari za kufanya manunuzi online
·         Huduma za usafirishaji (shipping services) na waranti.
 Pia ni jambo muhimu kuangalia kama kuna huduma ya usafirishaji, la sivyo, unaweza nunua vitu na bado ukahitajika kutoa gharama nyingine kuvileta ulipo!. Unapotaka kununua vitu kwa njia ya mtandao, inakubidi kuangalia tovuti tofauti tofauti kwa  kuwa zinatofautiana kwenye ubora wa huduma, mfano kampuni moja yaweza uza kitu (item) bila ya waranti (warranty), lakina nyingine yaweza uza pamoja ya kutoa waranti ya bidhaa, yaani product warranty!

NJIA ZINAZOTUMIKA

Credit card
Njia ya kawaida ya kununua vitu online ni kutumia credit kadi. Hii ni njia kubwa ya kununua vitu online au vitu dukani, ebooks online au bidhaa ambazo si rahisi kuzipata maduka ya rejareja . Wakati wa kununua kitu na credit kadi ni lazima kuhakikisha kwamba tovuti ni salama. Kawaida, tovuti itakuwa na lock kidogo juu yake pia huwa na kiungio cha https badala ya http!.

PayPal
Njia ya pili ya kawaida kwamba watu kununua vitu online ni kupitia PayPal. PayPal ni moja ya makampuni makubwa yanayotuo huduma ya kununua vitu online. Kama tovuti ni salama na halali, itatoa njia ya PayPal kama njia ya kuwasilisha malipo. Kufungua akaunti PayPal ni bure na rahisi sana. tembelea tovuti hii https://registration.paypal.com/na unaweza kuanza haraka.

eCheck
Moja ya njia ya kawaida kwamba watu kununua kitu online ni kupitia eCheck. ECheck inamuwezesha mteja wake kuchukua fedha na kuangalia salio. Akiba katika akaunti ya eCheck yaweza kutumika kufanya manunuzi online. Kama unatumia eCheck, kuwa na uhakika kwamba tovuti ni salama. Njia hii kuchukua muda mrefu sana kwa mchakato kuliko kadi za credit, na unaweza kusubiri kwa muda wa hadi siku saba kwa ajili ya malipo kufanyika.

Umuhimu:
Kununua huduma  na bidhaa online ni njia kubwa ya kuokoa  fedha na muda. Ni njia ambayo waweza nunua bidhaa kama za kielektroniki, vitabu na bidhaa za urembo!.

Angalizo:
Njia hii ya kufanya manunuzi online yafaa kutumika kwa tahadhari kubwa!, hakikisha unaona kiungio cha https://, badala ya http//, pia kiwe na alama ya kofuli kwenye address bar , mfano https://www.buyingstuffs.com,  vile vile usitumie njia ya manunuzi isyotambulika/hakikishwa kimataifa au kitaifa! Hakikisha kampuni unayotaka kununua vitu inatambulika na pia soma masharti na vigezo (terms and conditions) ili ujue kama uko salama kufanya nao biashara!

Umekaa nyumbani unataka kununua bidhaa zako lakini hujisikii kwenda duka lolote la jirani au ‘supermarket’. Usiwaze, mambo siyo kama zamani tena.
Watu wengi hawajui kuwa kupitia simu yako ya mkononi, tabiti, au kompyuta yenye mtandao, unaweza kununua bidhaa zako na kuzipata kwa muda mfupi mlangoni kwako.
Kasi ya ukuaji wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) imefungua milango ya kununua bidhaa mtandaoni kwa kuyavuta maduka na kupunguza utegemezi wa kununua bidhaa kwa kuonana na muuzaji.
Kampuni kadhaa za nje na za ndani kama Kaymu, Hellofood, Kivuko, Jumuia, ShoppingTz na nyinginezo, zimeanzisha huduma hiyo ili kutumia fursa adhimu ya biashara katika jamvi la Tehama.
Biashara hii inafanyikaje?
Katika soko au duka la mtandaoni, mteja na muuzaji hawakutani ana kwa ana, bali kupitia mtandao kwa kuunganishwa kupitia tovuti au programu ya simu (‘app’) ambazo nyingi humilikiwa na kampuni za kijasiriamali.
Tovuti hizo huwa ni jamvi au meza ambazo wauzaji huweka taarifa zao za kina kama vile bei na aina ya bidhaa, idadi, kiwango, mwaka wa kutengenezwa (kwa bidhaa za kuisha muda) na uwezo wake.
Taarifa hizo huambatana na picha halisi za bidhaa ili kuzuia utata unaoweza kutokea mteja anapokuta bidhaa aliyonunua na kuletewa siyo ile iliyopo pichani. Programu ya kompyuta inayofanya kazi kama kikapu hutumika kufanikisha ununuzi kwa kumjulisha mnunuzi jumla ya bidhaa alizonunua na fedha anazodaiwa.
Katika tovuti hizo kuna kila aina ya bidhaa kuanzia nguo, vyakula, magari, vitabu, vifaa vya elektroniki, vipodozi, vidani, muziki, video na vinginevyo.
Malipo
Malipo katika biashara hiyo iliyoanzishwa miaka 35 iliyopita na mjasiriamali Mwingereza Michael Aldrich, yanaweza kufanyika moja kwa moja mtandaoni au wakati mteja anapopokea bidhaa.
Meneja Mkuu wa kampuni ya kuuza chakula mtandaoni, Sherrian Abdul anasema wateja wanaweza kulipia kupitia Tigo Pesa (kwa sasa) au kulipia wakati wanapokea chakula.
Pia, shoponlinetz kupitia tovuti yao wamebainisha kuwa wateja wanaweza kufanya malipo yao kupitia kampuni za malipo za Visa, Visa Electron, Paypal, Mastercard, Airtel Money na Tigo pesa.
Bidhaa kama muziki na video au programu za kompyuta unaweza kuzipakua haraka mara tu baada ya kuzilipia, wakati bidhaa kama nguo na nyinginezo zitakuhitaji usubirie kidogo inatokana na umbali wa duka lilipo na makazi yako.
Changamoto za usafirishaji bidhaa
Pamoja na mfumo wa kielektroniki kufanya miamala ya biashara husika mtandaoni kwa haraka, usafirishaji wa bidhaa hadi kwa wateja umekuwa ukikumbwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa anuani za makazi. “Mara nyingi tunajitahidi kupata taarifa za msingi alipo mteja jinsi iwezekanavyo, mara nyingi tunaangalia mwanzo wa mtaa au kituo cha basi.
Ila tunategemea sana kampuni bora za usafirishaji kukamilisha zoezi hilo ambazo huwapigia wateja na kuwapelekea wateja bidhaa ndani ya muda unaotakiwa,” anasema Mkuu wa masoko na uhusiano wa Kampuni ya Kaymu, Angaza Nkurlu.
Hata hivyo, gharama za usafirishaji zinatofautiana kutokana umbali na ukubwa unaosafirishwa, kwa Kaymu bei hizo ni kati ya Sh3,000 hadi 4,000 kwa bidhaa ndogo ndogo na umbali wa kawaida wakati Hellofood ni kati ya Sh2, 000 hadi Sh3, 000.
Mustakabali wa biashara
Mtaalamu wa Tehama, Jumanne Mtambalike anasema biashara hiyo inakuwa kwa kasi huku kampuni za kimataifa kama Kaymu na Jumia zikibisha hodi nchini na kampuni za kizawa za Kivuko, Online Shopping na Gateway na nyingine nazo zimeonyesha ushindani mkubwa. “Unajua kati ya mwaka 2011 hadi 201,3 biashara za aina hiyo zilikuwa zinafanyika kupitia mitandao ya kijamii kama Facebook kwa muuzaji kuweka bidhaa anayouza kwenye ukurasa wake au wa kundi na kuweka mawasiliano ili wateja wanaohitaji wamtafute.
“Lakini mwaka huu tumeshuhudia tovuti lukuki maalumu kwa biashara hiyo na kwa taarifa nilizopatiwa hivi karibuni, mtandao wa Kaymu Tanzania unafanya biashara na watu zaidi ya 1,000,” anasema.
Licha ya biashara hiyo kukua kwa kasi nchini, baadhi ya wananchi kama Thabiti Ibrahimu hana uhakika kwamba ununuaji wa bidhaa mtandaoni una usalama wa kutosha hususan kwenye malipo.
Matukio ya wizi wa mtandao kupitia mashine za kutolea fedha au fedha kupitia njia ya simu, anasema yanazidi kumpa hofu iwapo kweli atapata bidhaa yake ikiwa salama.
Hata hivyo, Mtambalike anasema ni lazima wengi wapate hofu kutokana kutomjua mtu anayewauzia, huku akiwatoa wasiwasi katika upande wa malipo kwa kuwa maduka mengi yanataka ulipe wakati unapokea bidhaa hivyo unaweza kuikataa iwapo umeletewa usiyoihitaji.
“Kwangu mimi vikwazo vikubwa ni vitatu: uelewa mdogo wa watu kuhusu biashara za mitandao, ukosefu wa mfumo ulio imara wa malipo na wenye ulinzi wa kutosha na usalama wa taarifa za mnunuzi na ukosefu wa mtandao baadhi ya maeneo ya Tanzania,” anasema mtaalamu huyo.
Kwa Nkurlu, changamoto zilizopo ni fursa yao kuwekeza zaidi kwa kutoa elimu kwa wananchi namna ya kununua na kuendelea kupeana utalaamu kati ya wasafirishaji na watoaji huduma kifedha ili kuboresha zaidi biashara hiyo.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...