» » Kigwangalla asitisha operesheni ya kuchoma makazi Loliondo

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamis Kigwangalla leo Ijumaa ametangaza kusitishwa operesheni zilizokuwa zinaendelea katika pori tengefu la Loliondo na ametaka mifugo yote inayoshikiliwa na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ambayo haijafikishwa mahakamani kuachiwa.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara katika mji wa Wasso Loliondo baada ya kukutana na kamati ya ulinzi na usalama na madiwani, Dk Kigwangalla amesema amechukua uamuzi huo ili kusimamia dhana na uhifadhi endelevu na shirikishi.

Amesema  wizara hiyo itaendelea kusimamia sheria za uhifadhi kwa kushirikiana na jamii na haitakubali watu wachache kuvunja sheria za uhifadhi.

"Kwa mamlaka niliyonayo kwa watendaji wote wa wizara walio chini yangu, natangaza kusitisha operesheni iliyokuwa inaendelea na kurejeshwa kwa wananchi mifugo yote iliyokuwa inashikiliwa na wahifadhi ambayo uamuzi wake, hausubiri Mahakama," amesema.

Waziri Kigwangalla pia aliagiza wataalam wa maji katika Halmashauri ya Ngorongoro, kushirikiana na wataalam wa hifadhi kutoa maeneo nje ya hifadhi ili mifugo ya wananchi ipate maji.

Hata hivyo, amesema ili kudhibiti mifugo ya nchi jirani, kuingia

katika maeneo ya hifadhi nchini, mifugo yote sasa inatakiwa kuwekwa alama na mifugo kutoka nje itakayokamatwa itataifishwa.

Waziri Kigwangalla amesema anataka mamlaka ambazo zipo chini yake, kurejea katika kazi ya msingi kuhifadhi na kupambana na ujangili badala ya kufanya kazi ya kuchunga mifugo inayokamatwa.

"Uchukuaji mifugo inawafilisi wananchi na inajenga uadui baina ya wahifadhi na wananchi...kuna mifugo inakamatwa inakaa muda mrefu katika hifadhi baadhi inakufa na mingine inachungwa hifadhini, jambo ambalo sio wajibu wa wahifadhi," amesema.

Akizungumzia mifugo mingine ya wananchi, iliyokamatwa maeneo mengine ya hifadhi nchini, Dk Kigwangalla alitoa siku saba kwa watendaji wa wizara yake kumpa mapendekezo ya namna bora ya kutatua tatizo hilo ili afanye maamuzi.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn news

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...