» » Kauli ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma baada ya Rais Magufuli "Kumtumbua"

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma wa zamani, Jordan Rugimbana amesema hakuna kilichobadilika kwake kwa sababu mtumishi wa umma ni kama askari ambaye hachagui uwanja wa kupigana vita.

Rugimbana aliyeachwa katika mabadiliko madogo ya wakuu wa mikoa yaliyofanywa na Rais John Magufuli amesema hayo leo Jumatatu Oktoba 30, 2017 alipokabidhi ofisi kwa mkuu mpya wa mkoa huo, Dk Binilith Mahenge.

Akizungumza kuhusu mabadiliko hayo, Rugimbana amesema, "Mtumishi wa umma ni kama askari, hachagii uwanja wa kupigana vita, kwa lugha nyingine hakuna kilichobadilika nipeni muda mtaelewa."

Amesema anakwenda uraiani lakini jukumu lake sasa litakuwa ni kulipa fadhila kwa Rais Magufuli kwa kumchagua kuwa miongoni mwa wasaidizi wake wa kwanza katika Serikali aliyoiunda mwaka 2015.

Rugimbana amesema anachomuahidi Rais ni kuwa atakuwa raia mtiifu, mwaminifu na ataendelea kuwa timu Magufuli.

Amewasifu wakuu wa wilaya akisema ni watiifu, wamekuwa wakiuliza na kupokea ushauri wanaopewa.

Kuhusu utendaji wake, Rugimbana amesema mchakato wa Serikali kuhamia Dodoma unakwenda vizuri.

Mrithi wake, Dk Mahenge amesema atasimamia na kufuatilia mambo yote yaliyofanywa na Rugimbana kwa sababu ni maelekezo ya timu aliyokuwa akifanya kazi nayo.

"Nitasimamia na kufuatilia yote uliyoyafanya kwa sababu ni maelekezo ya timu yako. Wewe ni hazina uendelee kutushauri," amesema

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Zitto Kabwe ampongeza Nyalandu

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...