» » Ahukumiwa Miaka 30 Jela Kwa Kumbaka Mwanafunzi

Mkazi wa Mtaa wa Mitandi Lindi Mjini, Mussa Hassan (35) amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela na kulipa fidia ya Sh1 milioni, baada ya kukutwa na makosa ya kubaka na kumpa mimba mwanafunzi wa miaka 13 aliyekuwa anasoma darasa la sita.

Akisoma hukumu hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa, Erasto Philly alisema Mahakama imemtia hatiani mshtakiwa kutokana na ushahidi uliotolewa na shahidi namba moja katika kesi hiyo ambaye ni mwanafunzi.

Hakimu Philly alisema mshtakiwa alitenda makosa hayo Agosti 2017, kwa kumbaka na kumpa mimba mwanafunzi huyo.

Awali, Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Emmanuel John aliiomba Mahakama kutoa adhabu kali kutokana na mshtakiwa kutenda kosa la kinyama tofauti na umri wake ikilinganishwa na wa binti.

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles