» » Waziri Mkuu leo atazindua mfumo wa uandaaji bajeti

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Jumanne Septemba 5 atazindua mifumo miwili itakayosaidia kuongeza ufanisi na kupunguza gharama wakati wa ufuatiliaji na uandaaji wa bajeti nchini.

Katika uzinduzi huo, mawaziri sita ambao wanafanya kazi na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) watahudhuria.

Kiongozi wa timu ya rasilimali fedha, Dk Gemini Mtei amesema uzinduzi huo utahudhuriwa na Waziri wa Tamisemi, George Simbachawene; Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango; Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (sera, bunge, kazi, vijana, na watu wenye ulemavu), Jenista Mhagama.

Ofisa Usimamizi Mwandamizi wa Fedha Tamisemi, Elisa Rwamingo amesema mfumo huo utatumika katika halmashauri zote 185. Amesema wakuu wa vitengo katika halmashauri wamepatiwa mafunzo ya utumiaji wa mfumo huo, ambao wataenda kuwafundisha watumishi wengine.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn news

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...