» » Tundu Lissu Aikana Habari ya Kualikwa Kwenye Mkutano wa Wanasheria Bingwa Duniani

Rais wa  (TLS) na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ameikana taarifa inayosambaa mitaani na kwenye mitandao ya kijamii kuwa amealikwa kwenye Mkutano wa Mawakili Bingwa wa sheria nchini Marekani na kusema yeye mpaka sasa hajapata mwaliko huo.

Tundu Lissu alisema hayo  jana baada ya kutoka mahakamani katika kesi yake ya uchochezi ambapo alisema kuwa hata yeye anaona taarifa hizo kwenye mitandao ya kijamii na kusema hajapata huo mwaliko na kudai anasubiri.

"Mimi mwenyewe nimesikia nimealikwa sehemu fulani wakili pekee barani Afrika bado nausubiri huo mualiko sijauona bado ila nimeusikia mtandaoni, sijui watu ambao huwa wanasambaza uongo kama huu inawasaidia nini, mimi naona inanipandisha 'chat' nisizo stahili mimi nataka nipande 'chat' nazostahili " alisema Tundu Lissu

Katika taarifa hiyo ambayo imesambaa sana kwenye mitandao ya kijamii  ilikuwa inasema kuwa Mwanasheria huyo wa CHADEMA ni wakili pekeee kutoka barani Afrika ambaye atahudhuria Mkutano wa Mawakili Bingwa wa Sheria nchini Marekani utakaofanyika katika Jiji la Washington DC siku ya Ijumaa ya tarehe 15/09/2017

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn news

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...