» » Mwanasheria Amtaka Rais Magufuli Asaini Hukumu ya Kumnyonga Hadi Kufa Kijana Aliyeteka Watoto na Kuwaua

Mwanasheria wa kujitegemea hapa nchini Alberto Msando, amemtaka Rais Magufuli kusaini hukumu ya kunyongwa hadi kufa kwa mtuhumiwa wa mauaji ya watoto waliotekwa mkoani Arusha Bw. Samson Peter ili iwe somo kwa wengine.

Kwenye Ukurasa wake wa Instagram Alberto Msando ameandika ujumbe wa kusikitisha kuhusu vifo vya watoto hao waliotekwa na miili yao kukutwa kwenye shimo la choo mkoani Arusha, na kusema kwamba tukio alilolifanya mtuhumiwa huyo ni la ukatili wa hali ya juu, na kwamba kesi yake iendeshwe kwa haraka iwezekanavyo ili ahukumiwe na kumpa adhabu kali ikiwemo kunyongwa hadi kufa.

"Samson Peter Mungu akuadhibu, yaani huyu wala siyo wa kukaa zaidi ya miezi sita na kesi ya utekaji na mauaji!! Hii iishe hata kesho!! Na Rais asaini adhabu ya kunyongwa mpaka afe!! Naomba akihukumiwa tu Mh. Rais atengeneze historia ya kusaini kunyongwa kwake!!!", aliandika Alberto Msando.

Mwanasheria huyo machachari na maarufu Tanzania aliendelea kwa kuwataka wakazi wa Arusha kujitokeza kwa wingi katika shughuli ya mazishi ya watoto hao, ili kuwapa faraja wafiwa.

Watoto waliofariki Moureen David na Ikram Salim miili yao iliokotwa jana katika shimo la choo ambako walitelekezwa, baada ya kutekwa na mtu aliyejulikana kwa jina la Samson Peter ambaye kwa sasa anashikiliwa na polisi, kwa tamaa za fedha

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn news

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...