» » CCM Wampongeza Mbunge wao wa CCM aliyekodi ndege Ya Kumsafirisha Tundu Lissu

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimempongeza mwanachama wake aliyejitolea kudhamini ndege iliyomsafirisha Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki, Tundu Lissu kwenda jijini Nairobi nchini Kenya kwaajili ya matibabu.

Katika taarifa hiyo, imesema kuwa wamechukua hatua hiyo ya kumpongeza Mbunge wa Jimbo la Mpendae, Salim Hassan Turky kwa kuonyesha upendo, utu na mshikamano na kuweka kando tofauti za kisiasa.

“Kwa dhati kabisa tunampongeza mwanachama wetu na mbunge wa Jimbo la Mpendae, kwa kuonyesha utu na kuweka kando itikadi za kivyama kumsaidia Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu,” amesema Polepole kupitia taarifa hiyo

Hata hivyo, Polepole ameongeza kuwa wameamua kumpongeza mbunge huyo kwa kuonyesha uzalendo wa hali ya juu, kwani katika matatizo ni vyema itikadi za kisiasa zikawekwa pembeni ili kuweza kutatua kile ambacho kinakuwa kinawakabili.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...