» » Zambia: Kuanzia Sasa Kila Mwananchi ni Lazima Apimwe UKIMWI, Sio Hiari Tena


SeeBait
Rais wa Zambia, Edgar Lungu, ametangaza kwamba wananchi wote wanaofika katika vituo vya afya vya serikali wapimwe virusi vya Ukimwi kwa lazima, wapatiwe ushauri nasaha na tiba.

Rais Lungu amesema, sera hiyo mpya inaenda sawia na agenda ya serikali ya kutokomeza virusi vya HIV nchini humo ifikapo mwaka 2030.

Katika tangazo hilo, kiongozi huyo amesisitiza umuhimu wa kulinda maisha ya wale walioathirika na wale ambao wako hatarini kuambukizwa virusi hivyo.

Amesema, licha ya sera hiyo kukiuka haki ya mtu kupima kwa hiari lakini akasisitiza kuwa hakuna mtu mwenye haki ya kuweka rehani maisha ya binadamu mwenzake.

Sera hiyo inakiuka muongozo wa Shirika la Afya Duniani, WHO, na Shirika la Ukimwi la Umoja wa Mataifa, UNAIDS, unaohamasisha watu kupima Vvu na kupata ushauri nasaha kwa hiari.

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn news

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles