» » Serikali yalipongeza Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC)


Serikali imelipongeza shirika la utangazaji la Tanzania(TBC) kwa kuendelea kurusha matangazo mubashara katika ziara  mbalimbali za viongozi hapa nchini ikiwemo ziara ya Rais wa Jamhuri Misri hapa nchini.

Pongezi hizo zimetolewa mapema hii leo jijini Dar es salaam na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan muda mfupi mara baada ya kuagana na Rais wa Misri katika uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere.

Amesema kuwa shirika hilo la utangazaji linafanya vizuri ambapo limekuwa likihakikisha kuwa kila tukio kubwa limekuwa likirushwa mubashara hivyo kuwafikia wananchi moja kwa moja kwa wakati muafaka.

“Niwapongeze sana TBC, kwani tangu jana tumekuwa pamoja kwenye mapokezi mpaka leo hii tena wakati wa kumuaga, hivyo hongereni sana na nampongeza mkurugenzi wa TBC kwa kazi nzuri anayoifanya,”amesema Samia Suluhu.

Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) limekuwa likihakikisha linarusha matangazo mubashara ili kuweza kuifikia jamii moja kwa moja, hivyo kufikisha ujumbe kwa muda muafaka

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn news

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles