» » Rais Magufuli: Ni Bora Njaa Kama Hamtaki Kufanya Kazi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameendelea kuwaonya Watanzania wenye tabia ya uvivu na kupenda kubweteka bila kujituma, huku akisema wakati wa utawala wake hakutakuwa na vitu vya bure.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo alipokuwa akihutubia wananchi wa wilaya ya Korogwe mkoani Tanga waliohudhuria uzinduzi wa kituo cha mabasi (Stand) wilayani humo, na kusema kuwa watu wanaopenda kukaa vijiweni bila kujishugulisha huku wakilalamika njaa na hakuna pesa, ni bora wafe na njaa.

" Wakati wa kukaa kwenye magenge na kupiga maneno umepitwa na wakati, mnakaa kwenye pool unasubiri vitakuja hakuna, vya namna hiyo nataka kuwaeleza havitakuja kwenye utawala wangu, mnakaa mnasubiri tuna njaa tunataka mtuletee, mimi njaa nafuu ikuue kuliko nikuletee chakula, kwa sababu kama mwenzako ana chakula wewe una njaa, hatuwezi tukavumilia vitu vya namna hiyo", alisema Rais Magufuli.

Rais Magufuli aliendelea kusema ni lazima awaeleze Watanzania ukweli kuhusu hilo, bila kujali kuchukiwa kwani atasimamia haki huu akiwa na dhamira ya kwenda mbele.

"Ni lazima niwaeleze ukweli, nafuu mnichukie lakini niwaeleze ukweli, lakini hata mkinichukia hata sura yangu wala haipendezi, lakini mimi nitasimamia haki ya kuwaeleza ukweli, tunataka twende mbele, tunataka tubadilishe nchi, serikali itafanya juhudi zake zote kuwasaidia Watanzania", alisema Rais Magufuli

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn news

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...