» » Maamuzi ya Mahakama kuu kuhusu dhamana ya Manji

Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam Leo imeyatupilia mbali maombi ya dhamana yaliyowasilishwa na   Mfanyabiashara maarufu Tanzania Yusuf Manji baada ya kukubaliana na mapingamizi yaliyowasilishwa na DPP.

Maombi hayo yametupiliwa mbali na Jaji Isaya Arufani.

Kabla ya kutupiliwa mbali, maombi hayo, Manji alisimama na kuieleza mahakama kukataa kuwakilishwa na Wakili Peter Kibatala kwa sababu za kisiasa.

Amedai, alipopeleka maombi ya dhamana alimpa maelekezo wakili Joseph Tedayo lakini alishangaa kesi ilipofika mahakamani hapo kwa ajili ya kisikilizwa maombi yake ya dhamana wakili Kibatala ndiyo alifika kumuwakilisha.

Kutokana na hayo, Manji ameiomba Mahakama mawakili, Alex Mgongolwa, Hudson Ndusyepo na Seni Malimi ndio wawe wanamuwakilisha katika maombi hayo.

 Hivyo DPP akiwakilishwa na mawikili Paul Kadushi na Simon Wankyo walidai kuwa, wamesilisha kiapo kinzani kupinga maombi hayo ya dhamana wakiwa na hoja tatu.

Hoja hizo ni kuwa, Mahakama Kuu haina mamlaka ya kusikiliza maombi hayo ya dhamana na kwamba yanapaswa kusikilizwa na mahakama ya kifisadi kwa kuwa mshtakiwa anakabiliwa na makosa ya uhujumu uchumi.

Ameongeza kiqa vifungu vya kisheria vilivyotumika kuleta maombi hayo siyo sahihi na pia hati ya kiapo iliyoambatanishwa  kuunga mkono maombi hayo ina dosari kisheria ambazo haziwezi kurekebishika.

Kadushi aliiomba mahakama kusikiloza kwanza mapingamizi ya DPP kabla ya kuanza kusikiliza maombi ya dhamana.

Hata hivyo Wakili Mgongolwa akiwakilisha jopo la mawakili wa Manji walikubaliana na mapingamizi ya DPP kuwa ni kweli yana msingi na maombi ya dhamana yanadosari.

Kufuatia kukiri huko, Kadushi aliiomba mahakama kutupilIa mbali maombi hayo ya dhamana.

Akitoa uamuzi, Jaji Arufani amekubaliana na mleta Maombi (Manji) kuwa hawakilishwi na Kibatala. Pia amesema mahakama kuu haina mamlaka ya kusikiliza maombi hayo hivyo ameyatupilia mbali.

Katika maombi hayo ya dhamana, Yusuf Manji anaiomba Mahakama Kuu itengue hati ya kunyimwa dhamana iliyowasilishwa na Mkurgenzi wa Mashtaka (DPP) kwa kuwa ana matatizo ya kiafya akisumbuliwa na matatizo ya moyo.

Kwa mujibu wa hati ya maombi hayo, Manji anadai kuwa anasumbuliwa na maradhi ya moyo  na kwamba ameambatanisha vyeti vya daktari katika maombi yake.

Katika kesi ya msingi,  Manji na wenzake wanatuhumiwa kukutwa na mihuri ya mbalimbali ya JWTZ isilivyo halali vyote vikiwa na thamani ya Sh. milioni 236.5.

Mbali na Manji, washtakiwa wengine ni,  Ofisa Rasilimaliwatu Deogratias Kisinda (28), Mtunza Stoo, Abdallah Sangey (46) na Mtunza Stoo msaidizi, Thobias Fwele (43)

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn news

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...