» » Marekani yasema haina uadui na Korea Kaskazini

Waziri wa maswala ya kigeni nchini Marekani Rex Tillerson amesema kuwa Marekani sio adui wa Korea Kaskazini

Image captionWaziri wa maswala ya kigeni nchini Marekani Rex Tillerson amesema kuwa Marekani sio adui wa Korea Kaskazini
Serikali ya Marekani haitaki mabadiliko ya utawala Katika Korea Kaskazini, waziri wa mambo ya nje wa Marekani anasema, huku hofu ikitanda juu ya mpango wa silaha wa Pyongyang.
"Sisi si maadui zenu, " Rex Tillerson alisema, na kuongeza kuwa Marekani ilitaka mazungumzo wakati mmoja.
Wakati huo huo seneta wa chama cha Republican alisema rais Trump alihisi kuanza vita na Korea kaskazini ni chaguo
Pyongyang inadai kuwa jaribio lake la hivi karibuni la makombora linaweza kushambulia magharibi mwa Marekani na zaidi.
" Hatutaki mabadiliko ya utawala, hatulengi kuuangusha utawala, hatutaki kuharakisha muungano wa eneo la Peninsula, hatutaki sababu ya kutuma wanajeshi wetu kwenye eneo lenu ," alisema Bwana Tillerson, akimaanisha mpaka baina ya Korea kaskazini na Korea kusini.
"Sisi si maadui zenu, sisi si tisho kwenu , lakini munatuwekea tisho lisilo kubalikana lazima tujibu."
Jaribio la pili la kombora la masafa marefu linaloweza kshambulia bara jingine (ICBM) siku ya Ijumaa, lililosherehekewa na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un, lilikuwa ni jaribio la hivi karibuni kutekelezwa linalokiuka marufuku ya Umoja wa Mataifa
Rais Kim Jong un alisema kombora la masafa marefu linaweza kushambulia eneo lolote la Marekani
Image captionRais Kim Jong un alisema kombora la masafa marefu linaweza kushambulia eneo lolote la Marekani
Majaribio ya hivi karibuni ya makombora ya masafa marefu ya Korea Kaskazini yamesababisha hofu kubwa juu ya tishio la serikali ya Pyongyang dhidi ya Marekani , na kuzingatiwa kwa haja ya kuzuwia shambulio lolote nchini Marekani.
Hilo ndilo alilokuwa nalo akilini rais Trump katika mazungumzo juu ya vita na seneta Lindsey Graham.
Makao makuu ya wizara ya ulinzi nchini Marekani Pentagon, yametoa taarifa za hivi karibuni juu ya hatua za kijeshi , lakini wakati huo huo wachambuzi wanasema kukabiliana na Korea Kusini itakuwa ni maafa.
Hilo limemfanya , Bwana Tillerson arudie kwa marefu kwamba Marekani haitaki mabadiliko ya utawala na kuongeza kuwa lengo ni kufanya mazungumzo, lakini ambayo hayana msingi kwamba Korea Kaskazini inaweza kuendelea kutunza silaha zake za nuklia
Serikali ya Pyongyang hata hivyo imekataa kata kata masharti ya aina hiyo.


Tuma picha/ habari what-sap 0769436440



tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn news

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...