» » Mahakama Kuu Yatupilia Mbali Tena Ombi la wale Wabunge 8 wa CUF aliotimulia na Lipumba

Wabunge wanane waliofukuzwa uanachama na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF, anayetambuliwa na Msajili wa vyama vya Siasa nchini, Prof Ibrahim Lipumba, jana waliondoka vichwa chini baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es salaam kutupilia mbali ombi lao la zuio la kupinga kuapishwa kwa wabunge wapya.

Uamuzi huo umetolewa na Jaji wa mahakama hiyo, Lugano Mwandambo baada ya kusikiliza hoja zote za pande mbili, ambapo amesema kuwa mahakama imetupilia mbali hoja za walalamikaji za kuweka pingamizi kutaka wabunge wapya wasiapishwe mpaka kesi ya msingi isikilizwe.

Aidha, Mwandambo amesema kuwa mahakama itasikiliza pingamizi la walalamikaji walilofungua kupinga kufukuzwa uanachama wa chama cha wananchi CUF na mwenykiti wao Prof. Ibrahim Lipumba.

Katika maombi yao walalamikaji wanaomba kutoapishwa kwa wabunge wanane walioteuliwa na kutangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuziba nafasi zilizoachwa wazi na wabunge hao kwa mujibu wa katiba.

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles