» » madiwani wengine, Chadema yapata pigo tena, ya kimbiwa

Madiwani watatu wa Chadema Manispaa ya Iringa wameamua kuachia nafasi zao kwa madai ya mwenendo mbaya wa chama.

Madiwani hao walichukua uamuzi huo baada ya kumwandikia barua ya kujiuzulu mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa. Madiwani ambao wamechukua uamuzi huo ni Baraka Kimata wa Kata ya Kitwiru na wawili wa viti maalumu; Husna Ngasi na Leah Mlelewa.

Wakizungumzia uamuzi huo, viongozi hao walisema kuwa wameamua kufanya hivyo baada ya kuchoshwa na mwenendo wa chama hicho.

Kimata alisema anaendelea na kazi zake nje ya siasa na kwamba, hatabaki na nafasi yoyote ndani ya chama hicho.

Alisema kuwa ushirikiano mdogo kati yake na mbunge wa jimbo hilo umemsukuma kuachia nafasi yake hiyo.

Kwa upande wake, diwani mwingine ambaye alikuwa katibu wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), Mlelewa alisema hatabaki na nafasi yoyote ndani ya chama hicho kama ilivyo kwa Kimata.

Madiwani wengine wa Chadema ambao walijiuzulu kutoka Jimbo la Arumeru Mashariki ni Anderson Sikawa, Emmanuel Mollel, Greyson Isangya na Josephine Mshiu pamoja na diwani wa Murieti, Credo Kifukwe.

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn news

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles