» » Marekani kuipa Ukrain silaha za kupambana na waasi


Haki miliki ya pichaREUTERSImage captionRais wa Ukrain Petro Poroshenko (wa pili kulia) akikutana na maafisa huko Donetsk mwezi Juni

Mjumbe mpya wa Marekani nchini Ukrian anasema kuwa Marekani inatathmini ikiwa itatuma silaha kusaidia wale wanaopigana na waasi wanoungwa mkono na Urusi.

Kurt Volker aliiambia BBC kuwa kuihami serikali ya Ukrain itabadilisha msimamo wa Urusi.

Alisema hafikirii kuwa hatua hiyo itakuwa ni uchokozi.

Ukrain: Urusi ilihusika na udukuzi wa mitandaoMapigano mapya mashariki mwa UkrainUkrain yakiuka onyo la Urusi na kufanya mazoezi ya kijeshi

Wiki iliyopita wizara ya mashauri ya nchi za kigeni ya Marekani ilizitaka pande zote mbili kusitisha mapigano mashariki mwa Ukrain.

"Silaha za kujilinda, zile ambazo zitaisaidia ukrain kujilinda na kuharibu vifaru kwa mafano, ambazo zitaizuia Urusi kuitisha Ukrain," bwana Volker aliiambia BBC.

Image captionEneo linalokaliwa na waasi nchini Ukrain

Alisema kuwa mafanikio ya kuwepo amani mashariki mwa Ukrain yanahitaji kile alichokitaja mchakato wa mazungumzo na Urusi.

Bwana Volker na mjumbe wa zamani wa Marekani kwenye Nato na aliteuliwa kwenye wadhifa huo mpya mwezi huu.

Trump aitaka Urusi kuwacha kuivuruga UkrainUrusi kuvuruga matangazo ya radio kutoka Ukrain kwenda Crimea

Umoja wa Mataifa unasema kuwa zaidi ya watu 10,000 wameuawa tangu mzozo wa Mashariki mwa Ukrain ushuke mwezi Aprili mwaka 2014 mara baada ya Urusi kulimega eneo la Crimea.

Mapigano hayo yamesababisha zaidi ya watu milioni 1.6 kuhama makwao.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...