» » Israel yaondoa mitambo ya kutambua chuma mjini Jerusalem


Haki miliki ya pichaREUTERSImage captionIsrael yaondoa mitambo ya kutambua chuma mjini Jerusalem

Israeli imeondoa mitambo ya kutambua chuma iliyosababisha utata mkubwa, ambayo ilikuwa imewekwa katika eneo takatifu mjini Jerusalem, ambalo waislamu wanapaita Haram al-Sharif na kwa wayahudi Hekalu la mlimani.

Maafisa wakuu sasa wanasema kuwa, mitambo mingine ya uchunguzi, itawekwa ambayo haitatizi pakubwa waumini wanaofika kwa maombi.

Ghasia zilizuka wakati polisi wawili wa Israel waliuawa tarehe 14 mwezi huu.

Israel ilisema kuwa mitambo hiyo ilihitajika kwa sababu watu walikuwa wakiingia na silaha katika eneo hilo takatifu.

Israel yaweka kamera za ulinzi eneo takatifu mjini JerusalemIsrael yafungua eneo takatifu JerusalemRais wa Palestina akata mawasiliano na IsraelAskofu aliyewapatia silaha Wapalestina dhidi ya Israel afariki

Lakini hatua hiyo ilichochea maandamano.

Ijumaa iliyopita wapalestina watatu waliuawa kwenye ghasia na vikosi vya usalama vya Israel, wakati maefu ya waandamanaji walifika eneo la Jerusalem mashariki na ukingo wa magharibi linalokaliwa na Israel.

Israel pia inasema kuwa wafanyikazi wake wote waliokuwa wakifanya kazi katika ubalozi wake ulioko Jordan, wamewasili nyumbani, akiwemo mlinzi wa usalama ambaye alihusika katika kisa cha hapo jana Jumatatu, cha ufyatulianaji wa risasi, ambapo raia wawili wa Jordan waliuwawa.

Haki miliki ya pichaREUTERSImage captionIsrael ilisema kuwa mitambo hiyo ilihitajika kwa sababu watu walikuwa wakiingia na silaha katika eneo hilo takatifu.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...