Wasichana saba waliojifanya kuwa Waislamu kwa kuvaa vazi la hijab wamekamatwa nchini Nigeria kwa kujaribu kufanya safari haramu ya barani Ulaya ,kulingana na maafisa.
Wasichana hao ni miongoni mwa watu 12 waliokamatwa na maafisa wa uhamiaji mapema wiki hii walipojaribu kuvuka mpaka kaskazini mwa jimbo la Katsina wakielekea Ulaya.
Mamlaka ya uhamiaji inasema kuwa wasichana hao saba wanatoka Kusini mwa taifa la Nigeria, na walivalia vazi la Kiislamu ili kuwasaidia kupita kwa urahisi katika mpaka katika eneo la kaskazini lililo na Waislamu wengi.
- Vazi la hijab linaweza kupigwa marufuku kazini Ulaya
- Kenya: Mahakama yawaruhusu wasichana wavae hijab shule
- Msomali M'marekani awania taji la bi Minnesota
- Mfuasi wa Trump amshambulia Muislamu Marekani
Baadhi ya waliokamatwa walinukuliwa wakisema kwamba walitaka kwenda Ulaya ili kutafuta ajira kutokana na hali ngumu ya maisha nchini Nigeria.
Wasichana hao baadaye walikabidhiwa kwa kitengo cha kukabiliana ulanguzi wa watu kwa uchunguzi zaidi.
Takriban watu 40 wamekamatwa katika kipindi cha miezi minne iliopita nchini Nigeria wakijaribu kuvuka na kuingia nchini Niger ili kuelekea Libya kupitia jangwa la sahara kabla ya kuabiri boti na kuelekea Ulaya.
Wakati huohuo zaidi ya watu 1000 waliripotiwa kurudi wenyewe nchini Nigeria kutoka Libya katika kipindi cha miezi mitano.
Tuma picha/ habari what-sap 0769436440
BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

